Habari za Punde

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe.Othman Masoud Awatembelea Wagonjwa na Vizuka Wilaya ya Unguja

 
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba ni wajibu kwa viongozi wa ngazi mbali kuwa karibu na wananchi katika kusaidia kujenga umoja na ushirikiano miongoni mwao hasa katika kipindi hiki cha mwenzi mtukufu wa ramadhani.

Mhe. Othman  ambaye pia ni Makau Mwenyekiti wa ACT Wazalendo upande wa Zanzibar, ameyasema hayo huko viwanja vya Kwabimtoro mjini Unguja baada ya kukamilisha siku ya kwanza ya ziara yake ya kutembelea wagonjwa na vizuka katika  majimbo mbali mbali ya Uguja na Pemba.

Aidha Mhe. Othman amesema pia pamoja na mambo mengine ziara kama hizo ni muhimu kwani zinasaidia sana viongozi kupata funzo kubwa la kufahamu hali na maisha ya watu yalivyo na kutafakari juu ya namna bora ya kuendeleza umoja.

Mhe. Othman paia amesema kwamba ziara hizo pia zinatoa nafasi kwa viongozi kusikiliza moja kwa maoja matatizo ya wananchi na kuweza kufahamu hivyo kuwezesha  kutafakari namna ya kutafuta mbinu za pamoja za kuyatatu.

Mhe Makamu amewataka wale weto waliopatwa na mtihani wa maradhi ya aina mbali mbali kuendelea kuwa na subra na kufahamu kwamba maradhi ni mtihgani kutoka kwa mola muumba ambayo hupewa wanaadamu ili wapate kumkumbuka mola wao.

Aidha ameahidi wale wote aliowatembelea kwamba serikali kupitia viongozi mbali mbali wapo pamoja nao katika kusaidina kutafuta tiba ya maradhi yao.

Mapema Katibu wa Haki za Binaadamu na Makundi Maalum wa ACT – Wazalendo Pavu Abdalla Juma, amesema ziara hizo ni muondelezo wa urithi muhimu kutoka kwa mtangulizi  wa Mhe, Makamu Marehemu maalim Seif Shariff Hamad amabazo alizifanya kila ifikapo mwezi wa ramadhani na zinasaidia sana katika kujenga umoja na mshikamanoo miongoni mwa wananchi na viongozi wao.

Naye Katibu wa ACT- Wazalendo Mkoa wa Mjini Magharib Mahamoudu Ali Mahinda, amasema kwamba chama hicho katika ngazi ya Mkoa wa Mjini kimeanzisha mfuko  maalum wa faraja kwa ajili ya kusaidia wenye shida na changamoto mbali mbali ambao utakua na mwendelezo wa ziara za kutembelea wagonjwa na wenye shida mbali mbali.

Nao wagonjwa mbali mbali waliotembewa wamemshukuru Mhe. Othman  kwa uamuzi wake huo na kusema kwamba mwendelezo wa ziara kama hizo zinaofanywa hasa katika kipindi cha mwezi mtukufu wa ramadhani zinasaidia sana kujenga umoja na pia kuongeza imani kati viongozi  na wananchi wao.

Mhe. Othman katika ziara hiyo ametembelea majimbo Chumbuni, Shaurimoyo, Amani , Magomeni , Kwahani, Mpandae, Jang’ombe, Kiwajuni na Malindi katika wilaya ya mjini Unguja ambapo kesho anatarajia kutembelea majimbo ya Mkoa wa  Kaskazini Unguja.

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha Habari leo tarehe 26, 03,2023.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.