Na.OMKR. Zanzibar.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa
Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba wazanzibar na wadau wengine
wa uchaguzi wa Zanzibar wanaendelea kuwa na wasiwasi na mashaka yanayoweza
kutokea kwenye uchaguzi mkuu ujao kama
yalivyotokea kwenye chaguzi nyengine.
Mhe. Othman ameyasema hayo ofisini
kwake Migombani mjini Zanzibar alipokutana na kufanya mazungunzo na Kamati ya
Amani inayoongozwa na Mufti Mkuu wa Zanzibar inayowashirikisha viongozi mbali mbali wa dini
ya Kiislamu na wakrito.
Mhe. Othman amesema kwamba suala
hilo linatokana na kuendelea kuwepo viashiria na vitendo vinavyokosesha haki
baadhi ya wananchi jambo amnalo ndio chanzo kikubwa cha kuvurugika kwa Amani
kabla na baada ya uchaguzi.
Amesema kwanzishwa kwa kamati hiyo
ni jambo jema lakini kinachohitajika ni kuwepo nia thabiti katika na dhamira ya
kweli ya kuyakabili mambo yote yanayoleta mkanganyiko wa Amani kwa watu wa
Zanzibar katika miongo mitatu ya uchaguzi uliopita.
Amesema kwamba Nchi mbali za Afrika
wamefanya iuchgazi licha ya kwamba vyama tawala na vilivyopigania uhuru na
ukombozi wa nchi zao wameshindwa na kuwapongeza walioshinda na nchi zikaendelea
kuwa na Amani pamoja na kuendelea kuongoza nchi kwa kutumia mfumo wa serikali
za umoja wa kitaifa kwa zaidi ya vyama kumi.
Mhe. Othman amefahamisha kwamba
tafauti ya wazanzibari inapadnikizwa wa
watu wanaodhani kwamba nchi hiyo sio ya wote bali inawahusu kundi ama watu
Fulani wenye mnalaka ya kwamba lazima wawe wao kwenye madaraka hata kama
wameshindwa.
Amesema kwamba kamati hiyo ya Amani
kwa maoni yake bado haijafanikiwa kwa sababu chanzo kinacholeta migogoro ya
Zanzibar ni kutokuwepo haki kwa watu kunyimwa haki zao ikiwemo suala la
vitambulisho.
Amesema ili kustawisha Amani kabla
na baada hya uchaguzi ni la zima kamati hiyo kujikita kwa kuyaeleza baya na
wazi wazi kwa viuongozi wote amabo ndio chimbuko la kuvunjika kwa Amani ya
Zanzibar kabla na baada ya uchaguzi.
Ameeleza kwamba hakuna ngombe
anayeweza kuchinjwa kwa mkiani na kwamba kama hiyo inapaswa kwenda na kuyaeleza kwa undani masuala ambayo jamii
na viongozi wa siasa wanaamini na kufahamu kwamba ndio chimbuko la kukosekana
haki ikiwemo mifumo ya tume ya uchaguzi sharia na viongozi waiso waaadilifu
katika kusimamia uchaguzi wa Zanzibar.
Amesemisitiza kwamba Amani ya
Zanzibar ni si sisasa bali ni uchumi kutokana na ukweli kwamba wawekezaji wengi
duniniani hasa kwenye nchi ya visiwa kama Zanzibar ambayo uchumi wake unategemea huduma Amani ni
jambo la kwanza linalozingatiwa na wenye fedha duniani kote.
Amesema kewamba jukumu namba mnoja
ni watu kuwa na fursa ya kufanya mambo yao kwa utulivu na kwamba inapokuwa
hakuna Amani hata majina ya watu yanabadilishwa wengine wakaitwa wakimbizi.
Ameitaka kamati hiyo kuhakikisha
kwamba wawafikia wadau mbali mbali na
kutumia maarifa yao na weledi alionao ili kusikia kutoka kwenye midomo yao
kufahamu chanzo halisi cha mizozo na kuvunjika kwa Amani ya Zanzibar ili kuweza
kufanikiwa dhamira na lengo la kuundwa kamati hiyo.
Mapema Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kaab akiyeongoza ujumbe huo amesema kwamba kamati hyo
iliyoundwa na viongozi wa dini katika pande zote kwa dhamira ya kujenga Amani
Zanzibar kabla na baada ya uchaguzi.
Kwa Upande wake Makamu Mwenyekiti
wa Kamati hiyo ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Wokfu na Mali ya
Amani Zanzibar sheikh Abdalla Talib
amesema kwamba kamati hiyo imeundwa kutokana na kuwepo histori ya
kuvunjika kwa Amani kwa vipindi vyote vya uchaguzi.
Mwisho.
Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa
Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha Habari Leo Ijumaa tarehe
02 Mayi 2025.
No comments:
Post a Comment