6/recent/ticker-posts

80m/- Kununulia Vigari vya Walemavu

Na Mwandishi Wete.
Zaidi ya milioni 80 zanatarajiwa kutumika kwa mwaka wa Fedha 2014/2015 kununulia vigari vya Watoto wenye Ulemavu wa Viungo Zanzibar ili viweze kuwasaidia hasawanapokwenda skuli.

Waziri wa Nchi Ofisi yacMakamu wa Kwanzawa Rais wa Zanzibar Mhe, Fatma Ferej,aliyasema hayo jana katika ukumbi wa baraza lawawakilishi chukwani,wakati akijibu suala la  nyongeza la Mwakilishi waJimbola Muyuni Mhe, Jaku Hashim Ayoub, alipotaka kujuwa Walemavu wa viungo wamekuwa wakipata wakati mgumu sana hasa kwaWatoto walemavu wanaosoma skuli kukosa usafiri wa kufikia skuli.

Alisema katika bajeti ya mwaka 2012/2013 Serekali ilitenga jumla ya shilingi milioni 13 huku bajeti ya mwaka 2013/2014 ilitenga shilingi milioni 200 na kununua vigari kwa ajili yawatu wenye ulemavu Zanzibar.

Aidha alisema hivi sasa Wizara yake imekuwa ikipita nyumba hadi nyumba ili kuweza kuwapatia watoto hao huduma hiyo sambamba na kuwataka jamii kuacha tabia ya kuwafisha watoto wenye ulemavu na badala yake kuwatoa nje ili waweze kusaidiwa.

Akijibu suala la nyongeza lililoulizwa na Mwakilishi wacViti Maalum Mhe.Raya Suleiman Hamad, alipotaka kujua ni kwa nini watoto wenye ulemavu wamekuwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kuuziwa vigari vya kutembelea.


Waziri Ferej alisema Serekali haiuzi baskeli wala haitouza bali hutoa bure kwa watoto hao

Nae Mwakilishi wa Tumbe Mhe Rufai Said Rufai, alitaka kujua jambo gani linasababishwa na ulemavu wa viongo wakati wakati akiulizasaulila nyongeza.

Waziri Ferej alisema kwa sasa Serekali haijafanya utafiti juu ya watu wenye ulemavu ila inasemekana mtu huzaliwa nao au hupata ajali.


Akitoa takwimwi za watu wenye ulemavu,Waziri Fatma Ferej, alisema jumla ya watu 9,502 wenye ulemavu wa aina mbalimbali kwa Unguja na Pemba ambapo kati ya hao wapo watu wenye ulemavu wa Ngozi,Uoni,Uziwi na Viongo.             

Post a Comment

0 Comments