BAADHI wajumbe wa mkutano mkuu wa chama cha wananchi
CUF wilaya ya Mkoani Pemba wakimsikiliza
Katibu mkuu wa chama hicho, Mhe: Maalim Seif Sharif Hamad, wakati
akizungumza nao kwenye mkutano huo uliambatana na uchaguzi mkuu wa wilaya,
uliofanyika Jimbo la Mtambile jana (picha
na Haji Nassor, Pemba)
KATIBU mkuu wa CUF Mhe: maalim Seif Sharif
Hamad, akizungumza na wajumbe wa mkutano mkuu wa wilaya ya Mkoani Pemba wa
chama hicho, ambao uliambatana na uchaguzi mkuu wa wilaya, uliofanyika Jimbo la
Mtambile jana (picha na Haji Nassor,
Pemba)
MWAKILISHI wa CUF Jimbo la Kiwani Mhe: Hija
Hassan Hija akitoa neno la shukuran, mara baada ya Katibu mkuu wa CUF Mhe:
maalim Seif Sharif Hamad, kufungua mkutano mkuu wa chama hicho wilaya ya
Mkoani, ulioambatana na uchaguzi (picha
na Haji Nassor, Pemba)
KATIBU wa CUF wilaya ya Mkoani
Pemba, Tahir Awesu akiwasilisha utekelezaji wa chama hicho, kwenye mkutano mkuu wa wilaya ya Mkoani
uliofunguliwa na Katibu mkuu wa CUF Mhe: Maalim Seif Sharif Hamad, ambao
mkutano huo uliambatana na uchaguzi (picha
na Haji Nassor, Pemba)
Na Haji Nassor, PEMBA
KATIBU mkuu wa Chama cha wananchi CUF
Zanzibar Mhe: maalim Seif Sharif Hamad, amewataka wajumbe wa mkutano mkuu wa
wilaya ya Mkoani wa chama hicho, wasikubali kununuliwa na wagombea nafasi mbali
mbali, na badala yake wawachague viongozi kwa kuwaona wanafaa.
Alisema
ni kweli wapo baadhi ya wagombea wa nafasi zinazogombewa wamekuwa wakimwaga
pesa kwa wajumbe hao, na endapo watazichukua na kisha kuwapa kura kutokana na
fedha hizo, waelewa kuwa chama kitaanza kudhoofika.
Maalim
Seif ametoa kauli hiyo jana Mtambile wilaya ya Mkoani Pemba, wakati alipokua
akifungua mkutano mkuu wa wilaya, ulioambatana na uchaguzi wa kuwachagua
viongozi mbali mbali akiwemo Katibu, Mwenyekiti na wajumbe wa mkutano kuu taifa
CUF taifa.
Alisema
ni vyema wajumbe hao kuwa makini na kujitenga mbali na wagombea wenye nia ya
kusambaaza fedha, kwao kwa ajili ya kuwapigia kura wakijua kuwa viongozi wa
aina hiyo hawana nia thabiti na chama.
Alieleza
kuwa ni vyema kuwachagua viongozi ambao ni wapiganaji wa kweli na ambao
wataweza mapambano na vyama vyengine katika uchaguzi mkuu ujao, ili kuendelea
kushika hatamu wa nafasi mbali mbali ikiwa ni pamoja udiwani, uwakilishi na
ubunge.
‘’Mimi
niwanasihi sana ndugu wajumbe wa mkutano huu, ambao ndio wapiga kura wa
kuwachagua viongozi, lakini muelewa kuwa mkiwachagua viongozi legeleg ndio
mnakidhoofisha chama, na mkiwa makini ndio kusema CUF inaweza kushinda hata
ngazi ya raisi’’,alifafanua.
Katika
hatua nyengine Katibu mkuu huyo wa CUF, amewataka viongozi ambao watachaguliwa kuvunja
makundi mara moja, wakijua kama wakiyaendeleza yanaweza kuleta mpasuko ndani ya
chama.
Alisema
wapo, baadhi yao hata baada ya kuchaguliwa huendelea na vikao haramu na makundi
kwa wajumbe waliodhani wamewapigia kura, ambapo ni vyema wakaelewa mwisho wa
makundi ni mara baada ya kutangaazwa mshindi.
Mapema
akiwasilisha utekeleza wa kazi za chama kwa kipindi cha miaka mitano ijayo,
katibu wa CUF wilaya ya Mkoani Tahiri Awesu alisema pamoja na mafanikio
yaliopatikana, zipo changamoto kadhaa ikiwa ni pamoja na uhaba wa vitendea
kazi.
Katika
hatua nyengine alisema taarifa ambazo chama wanazo, kuna vitambulisho vya
uzanzibari ukaazi zaidi ya 4000 katika wilaya ya mkoani havijachukuliwa, hivyo
ametoa wito kwa wananchi kuvifuatilia.
Mapema
mwakilishi wa Jimbo la Kiwani Mhe: Hija Hassan amemuomba katibu mkuu huyo wa
CUF akiwa pia Makamu wa kwanza wa rais kufuatilia kwa karibu taarifa za kutaga
kupunguzwa tena majimbo kisiwani Pemba.
‘’Mimi
kama mwakilishi nnazo taarifa kwamba tume ya uchaguzi ya Zanzibar, inataka
kuyapunguza tena majimbo Pemba kutoka 18 ya sasa na kuwa 15, hili makamu wa
kwanza tunaomba lisifanyike, maana sisi CUF wilaya wala
hatutoliridhia’’,alifafanua.
Mkutano
huo mkuu wa wilaya, unatarajia kuwachagua katibu, mwenyekiti pamoja na wajumbe
wa mkutano mkuu taifa ambapo awali viongozi waliochaguliwa miaka mitano
iliopita walijiuzulu.
2 Comments
maalim nimeskia unagombea tena ukatibu mkuu mm ushauri wangu waandae watu wakuvaa viatu vyako mapema bila hivo kuna vita vya uongozi vinakuja ukija kuwa hupo tena maana sisi ni binaadam
ReplyDeleteAnonymous1 Nafikiri ushauri wako ni Mzuri sana lakini naona Wazanzibari wenyewe sio wajinga tena.. hawatachagua Mtu ambae ana onyesha kuwa na Dalili za Unafiki na Kuwagawa wazanzibari..Maalim Amechukua tena nafasi hiyo kwakuona kwamba kuna njama kubwa zakutaka kuwagawa wazanzibari katika dhama zilizopita.. Wazanzibari wanafaa kushukuriwa na hao viongozi wanaoipinga GNU, baada yakupiga kura za Ndio kwa asilimia 66% kukuba Umoja .Sasa Wazanzibari tumeweza kuwajua wale waliokua wapinzani wa umoja huo.. wanakusanyana kwa makundi kwenda mikutanoni ati wanasema Wawakilishi wanakwenda kuratibu Ilani za CCM.. Na wanatumia magari na hela za walipa kodi kwa mikutano hiyo..
ReplyDelete