6/recent/ticker-posts

TRA Yashauri Kuanzishwa Mtaala wa Kodi .

Na Mwandishi Wetu.
Serekali imeshauriwa kulipa kipaumbele suala la uazishwaji wa mitaala ya Kodi  kufundishwa katika skuli ili kuweza kutoa fursa kwa wanafunzi hao kuwa na uelewa wa mapema juu ya umuhimu wa kulipa kodi.

Hayo yameelezwa na Afisa wa Elimu kwa Walipa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Ndg Saleh Haji wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huko Ofisini kwake Mlandege mjini Zanzibar.

Alisema hatua hiyo pia itaweza kupunguza migogoro kwa wanajamii, kutokana na kuelewa maana ya kulipa kodi kwa wanafunzi hao.

Aidha alisema tofauti iliopo sasa ni miongoni mwa wafanyabiashara na Mamlaka za ukusanyaji wa mapato imetokana na kutokuwa na uelewa wa mapema juu ya haki hiyo kama raia wa nchi badala yake kuona Serekali ina lengo la kuwaharibia biashara zao, wakati wanapofuatilia kodi hizo.

’’Tutahakikisha tunaelimisha wanafunzi wote ili kila mmoja ajue umuhimu na maana ya ulipaji kodi ili hapo baadae isijekuwa ni tatizo ndani ya jamii,’’alisema ofisa huyo.


Aidha alifahamisha katika kuhakikisha wanafunzi hao wanaweza kutambua maana ya ulipaji kod, wamefanikiwa kuazisha klabu za kodi katika skuli ya Haile Ssalase pamoja na Skuli ya  Mombasa Biashara kwa lengo la kuwapa elimu ya kodi.

Ofisa huyo alisema kuwa endapo fursa hiyo itatolewa kwa skuli zote za Unguja na Pemba wataweza kuwajengea uelewa kwa haraka zaidi.

Alisema itakuwa vyema zoezi hilo kuendelezwa ili jamii iwe na elimu ya kutosha juu ya suala zima la ulipaji ili hapo baadae kusijekuwa na vikwazo ambavyo vinaweza kuleta mgogoro kati ya mlipa kodi na Mamlaka hiyo.


Post a Comment

0 Comments