6/recent/ticker-posts

Vigezo Ukuaji wa Uchumi Zanzibar Vyatajwa.

Na Mwandishi Wetu.
Serekali ya Mapinduzi Zanzibar  imesema itahakikisha kuwa inazingatia mambo matatu makuu katika ukuaji wa uchumi wa Zanzibar.

Mambo hayo ni pamoja na kutilia mkazo ukusanyaji na udhibiti bora wa mapato ili kuhakikisha malengo yaliokusudiwa yanaweza kufikiwa kwa wakati na kwa kiwango kilichokusudiwa.

Waziri wa fedha Mhe. Omar Yussuf Mzee, aliyasema hayo katika kikao cha baraza akijibu hoja za Wajumbe mbalimbali walizozitoa wakati wakichangia  bajeti kuu ya Serekali ya Mapinduzi Zanzibar ya mwaka wa fedha 2014/2015.

Waziri huyo alitaja jambo jingine ambalo Serekali inakusudia kulizingatia katika ukuaji wa Uchumi wa Zanzibar ni uibukaji wa vyanzo vipya vya mapato ambavyo vitaweza kuleta tija na manufaa katika ukuwaji wa uchumi.

Sambamba na hilo lakini Waziri huyo alisema Serekali itasimamia utulivu na kutilia mkazo suala la kuwepo kwa amani Zanzibar, hasaikizingatiwa kwamba suala la amani ndio nyezo muhimu katika kuimarisha hatua za kimaendeleo nchini.

Eneo jengine ambalo litasimamiwa ni kubaini wanaokwenda kodi na kuhakikisha wanafuata utaratibu wan a sheria za ulipaji kodi. Alisema.

Kuhusu Bajeti alisema Serekali imekuwa ikipata msaada wa asilimia 4.5 wa bajeti kutoka kwa wafadhili kila mwaka.

Waziri Omar alisema serekali kwa kuona umuhimu wa wafanyakazi hususani wataalamu, imeimarisha viwango vya mishahara kwa lengo la kuhakikisha wataalamu hao wanaendelea kutumikia nchini hasa katika sekta ya Afya na Elimu.


Pamoja na hayo alisema hatua nyegine ambayo serekali imekusudia ni pamoja na kuhamasisha wawekezaji kuazisha viwanda nchini kwa lengo la kupanua zaidi masuala ya kibiashara ambayo yataweza kutoa fursa za ajira kwa vijana.

Akizungumzia suala la Mikopo ya nchi ambapo baadhi ya wajumbe walitaka ufafanuzi kuhusu madeni ya nchi na athari zake kiuchumi, alisema kukopa sio kuteremka kwa uchumi wa nchi kwani hata nchi zilizoendelea zimekuwa zikikopa, ila suala la msingi ni kuzingatia mikopo hiyoitumike kwa masuala ya kimaendeleo ambayo yatakuwa yanainua uchumi wa nchi.

Akijibu hoja kuhusu suala la utegemezi alisema kwamba linaweza kuondoa uwepo wananchi wataendeleaza umoja na kuondokana na suala lakubaguana wenyewe kwa wenyewe.

Alisema kodi zinazokusanywa zinawanufaisha wananchi wote kupitia sekta mbalimbali ambazo kodi hizo hutumika katika masuala ya kimaendeleo.


Wakati akijibu hoja kuhusu namna ya kuisaidia sekta ya huduma, waziri alisema kwamba serekali inakusudia kuangalia upya namna ya kuipanua sekta hiyo ili iweze kuleta tija zaidi kwa uchumi wa nchi.       .             

Post a Comment

0 Comments