Hii ni timu machachari ya Kundemba ya miongo mitatu iliyopita ilikuwa ikicheza Central na hatimae daraja la pili. Picha hii ilipigwa mwaka 1984
Kutoka Kulia waliosimama ni Ahmed Nyenye ( Dila nene), Zahran Muazini, Ali Rajab, Ali Juma ( Yupo UK) Ramadhan Hassan ( Manishai), Ali Tall, Juma Sumbu ( Sasa ni Kocha). Waliokaa kutoka Kulia Muhsin, Juma Mkambi, Shaaban Mnyepe, Edi Abushiri, Juma Kikoti ( Marehemu) na Ali Jae ( Yupo UK)
Una kumbukumbu yoyote ya chama hili ambalo lilikuja kufutwa mwaka 1998 baada ya game kati yake na Mwera Star baada ya kutokea fujo uwanja wa fuoni iliyopelekea askari kuingilia kati kwa refa kuipendelea timu ya Mwera dhahir shahir.
Imerudishwa tena miaka miwili iliyopita na majuzi tu ilishuka daraja kutoka daraja pili na kuwa la tatu.
Mbunge Ummy Mwalimu alivyoleta tabasamu kwa bodaboda Tanga kupitia leseni
za udereva
-
Na: Dk. Reubeni Lumbagala, Tanga
Usalama wa maisha ya binadamu ni jambo la msingi sana, na ndiyo maana
unapaswa kulindwa kwa gharama zote. Katika suala la...
9 hours ago
No comments:
Post a Comment