Habari za Punde

Ujumbe wa Makunduchi waendelea na ziara yao nchini Sweden

 Picha ya pamoja na Meya wa mji wa Kiruna bi Christina. Picha hii imepigwa afisini kwake. Picha ya nyuma ya kuchorwa na picha ya meya aliyepita ambaye alifanya ziara Makunduchi wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. Kwa mujibu wa utamaduni wa Kiruna meya anayemaliza muda wake picha inayowekwa afisini ni ile ya kuchorwa
  Diwani wa Mzuri Kaja Makunduchi, Bi Zawadi Hamdu Vuai akimvisha Meya wa Kiruna Bi Christina kanga ya kisutu. Hii ni kuonyesha heshima ya Zanzibar



 Mfanyabiashara wa Kiruna bwana Mats ambaye ameonyesha hamu kubwa kuja Makunduchi kuwekeza katika hoteli. Katika mazungumzo alisema anapenda kufanya biashara zaidi kuliko kuoa



KUTEMBEA NI CHUO KIKUUNA MOHAMED MUOMBWA KUTOKA KIRUNA SWEDEN
Ziara ya ujumbe wa wadi za Makunduchi katika Manispaliti ya Kiruna nchini Sweden inatoa mafunzo mengi kwa Wazanzibari, kati ya mafunzo hayoni ubunifu ni mali na mambo mengi yanawezekana tukijipanga vizuri.
Safari ya madiwani wa Makunduchi wakiongozwa na Afisa tawala ndugu Abdallah Kombo nchini Sweden imekuja kufuatia makubaliano ya awali yaliyofikiwa ya mashirikiano kati ya manispaliti ya Kiruna na wadi za Makunduchi.
Pande hizo mbili zimekubaliana kushirikiana katika mambo ya utalii unaojali mazingira pamoja na elimu. Lakini mashirikiano haya hayakujatu kama mvua. Hapa ndipo ule usemi usemao hakuna kisichowezekana unapofaa.

Wadi za Makunduchi baada ya kutafakari zimegunduwa kuwa katika ulimwengu huu wa utandawazi kazi ya kuunganisha nchi kwa nchi si lazima kufanywa na balozi.
Kwa lugha nyengine diplomasia katika karne ya utandawazi sio milki tena ya mabalozi na ndio maana wadi za Makunduchi zikaamua kutafuta ushirikiano na sehemu moja wapo ya nchi ya Sweden. Matokeo ya jitihada hizi zilizoendeshwa kwa mawasiliano ya mtandao ni kuzaliwa kwa mashirikiano baina ya Manispaliti ya Kiruna n awadi za Makunduchi.
Ujumbe wa manispaliti ya Kiruna ukiongozwa na bwana Ove ulifanya ziara ya siku nne Makunduchi wakati wa kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Ziara hiyo ilikuwa na lengo la kuona maendeleo yetu kielimu na utalii kwa jumla ili kupata picha kamili ya namna nzuri ya kushirikiana.
Wakati wana Kiruna wakiwa Makunduchi, pamoja na mambo mengine, walitembelea sehemu ya ukanda wa utalii Paje, Bwejuu na Jambiani kwa upande wa Kusini. Kwa upande wa Kaskazini walitembelea Nungwi na Kiwengwa.
Jambo jengine lililopelekea wadi za Makunduchi kutoka nje ya mipaka yake ni kuitikia wito wa Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohammed Shein unaoutoa kila siku kuwa wakati umefika wa watu wa Zanzibar kuachana na tabia ya kufanya kazi kwa mazoea. Kwa lugha nyengine rais wa Zanzibar anawataka wananchi kuwa wabunifu katika utendaji wao wa kazi.
Mambo yalikuwajee ziarani Kiruna? Wazanzibari wanayo mambo mengi ya kujifunza kama wanatak akujikwamua kimaendeleo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.