Na Kauthar Abdalla
MJUMBE
wa Baraza Kuu la Uongozi la CUF, Ismail Jussa Ladhu amesema Zanzibar
itakapoanza kuchimba mafuta na gesi,uchumi wake utaimarika na kufikia wa nchi
ya Qatar
ambayo wastani wa pato la mwananchi kwa mwaka ni dola za Marekani 21,000.
Akiwahutubia
wanachama wa chama hicho katika viwanja vya Masumbani,jimbo la Chumbuni,Jussa
alisema inashangaza kuona serikali ya Muungano inaiwekea ngumu Zanzibar
katika suala la mafuta na gesi asilia,wakati upande wa Tanzania Bara wananufaika.
Alisema
nchi ya Qatar ambayo haina mafuta, isipokuwa gesi uchumi wake umebadilika na
kuwa nchi tajiri katika falme za kiarabu.
Jussa
ambae pia ni Mwakilishi wa jimbo la Mji mkongwe alisema sehemu kubwa ya utajiri
wa nchi unatokana na viwanda hivyo kutokuwepo kwa viwanda Zanzibar ndio sababu kuu ya kuathirika kwa
maeneo ya uchumi.
Aidha
alisema suala la mfumko wa bei za bidhaa nchini unaongeza viwango vya riba kwa
mabenki kwani uchumi wa kisiwa ni wa kutoa huduma kwa watu wanaopita
kibiashara.
Hata
hivyo, alisema serikali inajenga mazingira mazuri pamoja na kusimamia sera na
sheria zilizopo ili wawekezaji waingie kwa wingi kwa kutambua kwamba mapato
mazuri ndio muhimili wa uchumi nchini.
Sambamba
na hayo pia alielezea kwamba ni muhimu kufanya kazi kwa pamoja kama nchi bila
kujali tofauti za vyama kwani ni vitu vya mpito na nchi itabaki kama ilivyo.
Pamoja
na hayo alisema endapo nchi haina utulivu hali ya wananchi iko mashakani ambapo
ajira na kipato kwa wananchi hakitakua katika kiwango kinachostahiki.
Juzi
Baraza la Biashara la Zanzibar lililokutana chini ya Mwenyekiti wake, Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk.Ali Mohamed Shein
lilizungumza kwa kina na kuliwekea maazimio suala la maendeleo ya viwanda kwa
uchumi wa Zanzibar.
No comments:
Post a Comment