Warioba:Katiba haipatikani kwa maoni ya upande mmoja
Na Mwandishi wetu, DSM
MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, ameonya kwamba hakuna katiba itakayopatikana kwa kusikiliza maoni ya upande mmoja.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Jaji Warioba aliyashauri makundi ya kisiasa yanayovutana yakutane kujadili kwa kina suala hilo na hatimae kufikia muafaka.
Alisema Watanzania wanahitaji katiba bora itakayohusisha mawazo ya makundi yote, hivyo wanasiasa wanapaswa kutafakari kwa pamoja badala ya kugawanyika.
Alisema huu si wakati wa kuvutana na malumbano badala yake ni wa kutafakari na kushauriana kwa pamoja ili Tanzania ipate katiba bora.
“Tunataka katiba bora itakayoridhiwa na Watanzania wote na sio kuanzisha malumbano yasiyo na msingi,” alisema.
Hata hivyo, alisema Tume itaridhia marekebisho ya sheria mabadiliko ya katiba yaliyopitiwa na Bunge baada ya kusainiwa na Rais.
MAREHEMU JENISTA MHAGAMA ALIKUWA KIONGOZI JASIRI,MWAMINIFU NA MLEZI WA
VIONGOZI WA WENGI - RASI DKT SAMIA
-
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan leo
ameongoza familia, viongozi, wabunge na waombolezaji katika ibada ya kuaga
mwi...
1 hour ago
0 Comments