Habari za Punde

Picha na matukio kutoka Pemba

 
WAANDISHI wa habari wengi wamekuwa wavivu wa kuandika habari za vijijini, na kuandika zaidi habari za misafara ya viongozi na semina, ambapo pichani waandishi wa habari, kushoto wakioongozwa na mwandishi wa kujitegemea, Omar Hassan wakiwa na Mwenyekiti wa jumuia ya ‘JAMBO GROUP’ ya Kwazani Wambaa Mkoani, wakiwa na zawadi za matunda, baada ya kuwafikia na kuawandikia habari (picha na Haji Nassor, Pemba)

WAPIGANAJI wa Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, wakimsikiliza Afisa mpiango wa kituo cha huduma za sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba Khalifan Amour hayupo pichani, alipokuwa akizungumza nao, kujua mafanikio na changamoto zinazowakabili, ambapo ujumbe wa ZSLC hujiwekea utaratibu wa kutembelea vyombo vinavyosimamia sheria kila mwaka (picha na Haji Nassor, Pemba)

 MKUU wa wilaya ya Wete Pemba, Omar Khamis Othuman, akifungua mdahalo wa wazi kwa wanajumuia za kiraia, ili kujenga mbinu ya kushirikiana na kamati za kudumu za baraza la wawakilishi, katika kujadili na kutoa michango yao katika miswada ya sheria, kulia ni Mwenyekiti wa PACSO Omar Ali Omar na kushoto ni mfafanuzi wa mada, Juma Bakari Alawi, mdahalo huo uliofanyika skuli ya sekondari ya Fidel castro (picha na Haji Nassor, Pemba)    
 
 
WANAFUNZI wanaokaa skuli ya sekondari ys Fidel castro Pemba, wakiwa katika harakati za kugawana mlo wa mchana skulini hapo, baada ya kukabidhi beseni ya chakula na muhusika wa chakula na kisha kujigawawiya wenyewe (piccha na Haji Nassor, Pemba)

MWALIMU Mkuu skuli ya maandalizi ya ‘STAR’ iliopo Kichungwani wilaya ya Chakechake Pemba, Moza Said Salum akimkabidhi mwanafunzi wake, ambae ni mshindi wa mchezo wa kuokota mbatata, uliofanyika ili kuwaaga wenzao waliomaliza elimu ya maandalizi, sherehe hizo zilifanyika uwanja wa tenis Chakechake (picha na Haji Nassor, Pemba)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.