Na
Masanja Mabula
MAHAKAMA
ya ardhi Zanzibar
bado inakabiliwa na upungufu wa mahakimu wa kuendesha kesi za ardhi sambamba na
ukosefu wa majengo ya kufanyia kazi.
Hali
hiyo imesababisha mrundikano mkubwa wa kesi za ardhi katika mahakama mbali
mbali Unguja na Pemba .
Jaji
Mkuu wa Zanzibar, Omar Othman Makungu, amesema kwa sasa Zanzibar ina jumla ya mahakimu watano wa
mahakama ya ardhi ambao hawawezi kukidhi haja ya kusikiliza kesi za ardhi zinazofikia
zaidi ya 1000.
Jaji
Makungu aliwaambia wasaidizi wa sheria wa majimbo wakati wa kongamano la
wasaidizi wa sheria wa maajimbo Tanzania
lililofanyika mjini Unguja.
Alisema
pamoja na idara ya mahakama kuchelewesha uamuzi wa kesi hizo, wasaidizi wa
sheria wa majimbo wanalo jukumu la kuwaelimisha viongozi wa serikali za mitaa
kutojihusisha na migogoro ya ardhi kwa kuwa viongozi hao ndio chanzo cha
migogoro hiyo.
“Tatizo
ni upungufu wa mahakimu wa mahakama hizo, kwani kwa sasa tunao mahakaimu watano
tu kwa Unguja na Pemba hivyo inawawia vigumu kuhudumu kusikiliza kesi zote
zinazoripotiwa,” alisema.
Aliwalaumu
viongozi wa serikali za mitaa wakiwemo masheha na madiwani kwa kujihusisha na masuala
ya kuuza ardhi, hivyo inakuwa vigumu kuweza kupatikana kwa ushahidi wa kesi
hizo mahakamani.
“Unajua
kiongozi wa serikali ya mtaa (sheha) unapomwita mahakamani kutoa ushahidi
anakwambia niko kikaoni kwa Mkuu wa wilaya au nimeitwa na Mkuu wa mkoa, hivyo
ushahidi unakuwa haupatikani,” alisema.
Hata
hivyo wasaidizi wa sheria wa majimbo waliitaka idara ya mahakama kuongeza
watendaaji wa mahakama ya ardhi ili kuzifanya kesi hizo zipatiwe uamuzi unaofaa
na kwa wakati.
No comments:
Post a Comment