OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 04 Julai, 2014
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amesema
visiwa vya Zanzibar vimeendelea kuvutia wageni wengi kutokana na utajiri mkubwa
wa historia yake na uthiri wa utamaduni wa watu wake pamoja na mazingira mazuri
ya kuvutia.
Akizungumza na
Mwanamfalme wa Japan Akishino pamoja mkewe Ikulu leo, Dk. Shein amesema pamoja
na visiwa vya Zanzibar kubahatika kuwa na fukwe maridadi zinazovutia watalii
wengi lakini nafasi yake katika historia iliyopelekea kutembelewa na watu
kutoka nchi mbali mbali ulimwenguni kwa karne nyingi imevifanya visiwa hivyo
kuwa maarufu hivyo kuendelea kuvutia wageni wengi.
Alimwambia
mwanamfalme huyo ambaye yuko nchini kwa ziara maalum kuwa historia ya Zanzibar imeunganika na
mataifa mengine ulimwenguni hivyo ni vigumu kuandika au kuzungumzia historia ya
watu wake bila kugusia mataifa mengine.
Alitolea mfano
mji mkongwe kuwa moja ya urithi wa uthibitisho wa makutano ya tamaduni kutoka
nchi mbalimbali hadi sehemu hiyo ya mji wa Zanzibar kuwa uthiri wa dunia chini ya
Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni ya Umoja wa matyaifa-UNESCO.
Katika
mazungumzo hayo Dk. Shein ameishukuru pia Serikali na wananchi wa Japan kwa
misaada mbalimbali ambayo imekuwa ikiipatia Zanzibar na ametolea mfano sekta ya huduma za
jamii na miundombinu.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi amempongeza
Mwanamfalme Akishino na mkewe kwa kuitembea Zanzibar
na amemueleza kuwa milango iko wazi kwa Mwanamfalme huyo kutembelea Zanzibar wakati wowote.
Dk. Shein
alieleza matumaini yake kuwa ziara hiyo ya Mwanamfalme huyo itafungua njia kwa
watalii wengi kutoka Japan kutembelea Zanzibar .
Kwa upande wake
Mwanamfalme Akishino amemueleza Mhe Rais kuwa ni mara yake ya kwanza kutembelea
Zanzibar na anatarajia kujifunza mengi kuhusu Zanzibar kwa kutembelea
sehemu mbalimbali.
Miongoni mwa
waliohudhuria mazungumzo hayo ni pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu
na Utawala Bora Dk. Mwinyihaji Makame, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa Mahadhi Juma Maalim,Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni,Utalii na Michezo Bi Hindu Hamad Khamis na Balozi wa Tanzania nchini
Japan Balozi Salome Sijaona.
Postal Address: 2422 Tel.+255
776 613 015, Fax: 024 2231822
Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana
na Mwana Mfalmewa Japani Prince Akishino alipowasili Ikulu mjini
Zanzibar leo akifuatana na Mkewe Princess Akishino na baadae kufanya mazungumzo
Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Dk.Ali Mohamed Shein (kulia)akifuatana na
Mwana Mfalmewa Japani Prince Akishino na Mkewe Princess Akishino mara
walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leoRais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto)akimuonesha kitu Mwana Mfalmewa Japani Prince Akishino baada ya mazungumzo yao alipotembelea Ikulu Mjini Zanzibar leo na Mkewe Princess Akishino,[Picha na Ramadhan Othman)
No comments:
Post a Comment