6/recent/ticker-posts

Wanaharakati Vijana Wakutana na Makamu wa Rais Dkt.Bilal Dar-es-Salaam.Vipaumbele vya MILENIA

Kutokana na utafiti mpya, zaidi ya watu bilioni moja watakabiliana na maisha ya umaskini uliokithiri kama viongozi hawatafanya maamuzi muhimu juu ya umaskini, kukosekana kwa usawa na mabadiliko ya hali ya hewa katika mikutano miwili muhimu ya New York na Paris baadaye mwakani.

Hiyo ni tahadhari iliyotolewa na zaidi ya taasisi elfu moja dunia nzima ambazo zimeungana kuzindua kampeni inayoitwa hatua/2015, zikiwataka viongozi wa kitaifa na dunia kuchukua hatua za haraka na madhubuti ili kuondoa mabadiliko ya hali ya hewa yanayosabishwa na shughuli za binadamu, kumaliza umaskini na kushughulikia swala la matabaka.

Mahesabu mapya yaliyotolewa na hatua/2015 yanaonyesha idadi ya watu wanaoishi katika umaskini uliokithiri-chini ya shilingi elfu mbili kwa siku-inaweza ikapunguzwa kutoka zaidi ya bilioni moja hadi milioni 360 ifikapo mwaka 2030.

Hata hivyo, kama viongozi watashindwa kuendeleza kasi iliyopo ya  mikakati ya maendeleo kwenye Mkutano Maalumu wa Umoja wa Mataifa juu ya maendeleo endelevu mwezi wa tisa na Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu mazingira mwezi wa kumi na mbili, na wakapunguza juhudi zao, watu wanaoishi katika umaskini uliokithiri wataongezeka hadi kufikia bilioni moja na laki mbili ifikapo mwaka 2030. Ongezeko hili litakuwa la kwanza kwa kizazi hiki toka mwaka 1993 na ni zaidi ya ongezeko la watu bilioni moja (milioni mia nane sitini na sita) ukilinganisha na kama hatua stahiki zingechukuliwa. Kwa hali hii, mmoja kati ya kila watu watatu duniani ataishi chini ya shilingi 2500 kwa siku.

Malala Yousafzai, mshindi wa tuzo ya Nobel ambaye aliweka maisha yake hatarini kwa sababu ya elimu anasema; 


“Mwaka 2015 ni lazima uwe mwaka wa dunia kuamka na kuhakikisha dunia salama na yenye haki kwa watoto na vijana. Wote lazima tupambane kuhakikisha hili linatokea. Usipoteze nafasi hii’’

Pamoja na Malala, watu wengine wanaharakati mashuhuri wakijumuisha Askofu Desmond Tutu, Mo Ibrahim, Angelique Kidjo, D’banj, Malkia Rania wa Jordan, Bono, Ben Affleck, Bill na Melinda Gates na Ted Turner wanaunga mkono muunganiko wa taasisi zaidi ya elfu moja kwnye nchi zaidi ya 120 duniani. Kampeni inatoa wito kwa viongozi wa dunia kukubaliana juu ya mipango ya ya kumaliza umaskini, kuzuia madadiliko ya hali ya hewa na kukabiliana na ukosefu wa usawa.

Hatua/2015 ambayo ilitangazwa na Malala wakati akipokea tuzo ya Nobel-ni moja kati ya kampeni kubwa zaidi zilizowahi kuanzishwa ikijumuisha mazingira, haki za binadamu, taasisi za maendeleo na jumuia za kidini. Kutoka kwenye makampuni maarufu kama Amnesty International na Save the Children, hadi taasisi za kampeni na utetezi kama ONE, hadi taasisi zinazofanya kazi na jamii, harakati hizi zinadhamiria kuhakikisha makubaliano ya mwaka 2015 yanaundwa na watu.

Kwa Tanzania, vijana wamekutana na Makamu wa Rais Mheshimiwa Dr Mohamed Gharib Bilal kwa majadiliano juu ya matarajio yao kwa ajili ya baadaye na hatua wanazotaka viongozi wao wa kisiasa wazichukue mwaka 2015.

Mmoja wa vijana hao, Eva, ambaye na miaka 14 anasema;

“Mwaka huu ninapotimiza miaka 15, viongozi watakubaliana juu ya mpango wa kuifanya dunia iwe bora zaidi. Kama wakifanikiwa kuifanya vizuri, na wakaisimamia, kwa hakika hapatakuwa na watu wenye umaskini uliokithiri popote duniani wakati ntakapokuwa nafikisha miaka 30. Ni maisha yetu ya baadaye yaliyo kwenye hati hati. Ndio maana mimi na maelfu wenzangu tunataka viongozi wetu wafanye maamuzi sahihi ifikapo mwaka 2015’’

Dr Sipho S. Moyo, Mkurugenzi Mtendaji wa ONE Afrika anasema;

“Dira ya maendeleo ya Tanzania ya mwaka 2025 ni kuitoa nchi kutoka kipato cha chini hadi kipato cha kati ifikapo mwaka 2015. Kwa hili kufanikiwa, sera sahihi zenye vipaumbele lazima ziwekwe ili kukabiliana na umaskini uliokithiri na kukosekana kwa usawa kwa kutoa fursa za kijamii kama elimu bora na kuwezesha mazingira ambayo Shirika la Kazi la Kimatifa linaita ajira yenye staha. Ni muhimu kwa hiyo serikali iende kwa kasi na kiufanisi katika kutekeleza mkakati  wake wa Matokeo Makubwa Sasa,  ambao unalenga katika kuongeza msisitizo na dhamira ya serikali katika kuondoa umaskini na njaa na hivyo kuufanya mwaka 2015 kuwa mwaka utakaoleta nchi hii karibu na mafaniko makubwa kwa kila mtu hapo baadaye’

Margaret Mliwa – Mkurugenzi Mkazi wa Restless Development anasema:
‘Uzinduzi wa hatua/2015 ni muhimu kwa vijana wa Tanzania, kwani unafungua njia ya majadiliano baina ya vijana na viongozi wao. Kwa hatua na juhudi za pamoja za kushinikiza maamuzi muhimu kwa mwaka 2015 ili kukabiliana na umaskini na ukosefu wa usawa, sote tunaweza kuifanya Tanzania mahali bora zaidi’
Kwa upekee kabisa, kwa hakika huu ni mwaka wa vijana wa Tanzania kuhamasika na kuhakikisha maamuzi yatakayofanywa na serikali yao yanawakilisha aina ya Tanzania wanayotaka kuiona.

Kama sehemu ya uzinduzi wa kampeni ya hatua/2015, shughuli tofauti zinaendelea kwenye zaidi ya nchi 50 duniani. Nyingi zinaongozwa na watoto wenye miaka 15-ambayo ndio sehemu kubwa ya watakaothirika na makubalino ya mwaka huu.


·        Nchini Uganda, vijana watazungumza na Waziri wa Mambo ya Nje kumtaka asikilize matakwa yao wakati wakimkabidhi mswada uliosainiwa na zaidi ya vijana 10,000
·        Nchini Nigeria, watoto wa miaka 15 watamuuliza maswali waziri wa fedha, Ngozi Okonjo-Iweala kwenye televisheni ya taifa
·        Nchni Afrika Kusini, vijana wa miaka kumi na tano kutoka nchi nzima watakutana na waziri wa Michezo, Fikile Mbalula katika mji wa kihistoria wa Soweto kumtaka ajiunge nao katika kuwaandalia mazingira salama kwa ajili ya kizazi chao.
·        Jijini New York, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki- moon atakutana na kundi la vijana wa miaka 15 kujadili kwanini wanahitaji dunia ichukue hatua mwaka 2015
·        Nchini Uingereza, baadhi ya wanaharakati vijana watakutana na Waziri Mkuu David Cameron na Ed Miliband, kiongozi wa Upinzani, kuwataka kuchukua fursa iliyopo mwaka 2015.

Hatua/2015 inatoa wito kwa wananchi kujiunga nao kuhakikisha viongozi wa dunia wanajikita kuboresha dunia. Mwaka 2015 kampeni itatoa fursa kwa yoyote na popote alipo kushiriki katika kushawishi matokeo ya majadiliano haya ya dunia ili kuweza:


      Kumaliza umaskini wa aina azote
      Kupata haki za watu za msingi, kumaliza matabaka na ubaguzi
      Dunia ambayo yeyote anaweza kushiriki na kuwawajibisha viongozi wake



Post a Comment

0 Comments