Habari za Punde

Kikosi cha Timu ya Sudan ya Al Hilal Yawasili Zanzibar kwa Mchezo wao na KMKM

Wachezaji wa timu ya Al Hilal ya Sudan wakiwa katika chumba cha mapokezi baada ya kuwasili leo kwa mchezo wao wa marudio na timu ya KMKM unaotarajiwa kufanyika uwanja wa Amaan mwishoni wa wiki hii. katika mchezo wao wa awali uliofanyika Nchini Sudan timu ya Al Hilal imeshinda 2--0 
Wachezajin wa Timu ya Al Hilal wakitoka katika jengo la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar baada ya kuwasili Zanzibar kwa ajili ya Mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika.. 
Wachezajin wa Timu ya Al Hilal wakitoka katika jengo la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar baada ya kuwasili Zanzibar kwa ajili ya Mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika.. 
Wachezaji wa timu ya Al Hilal wakisalimiana na Wananchi wa Sudan walioko Zanzibar wakifanya kazi walipofika kuwapokea uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume kwa ajili ya mchezo wao wa marudio na timu ya KMKM. 


Kocha wa timu ya Al Hila  Al Patin Nagah,akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali walioko Zanzibar kuhusiana na timu yake kuhusiana na maandalizi ya mchezo wao wa marudiano na timu ya KMKM unnaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa wiki hii katika uwanja wa amaan Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.