Na
Mwandishi wetu,
Timu
bingwa ya michuano ya mei mosi iliyofanyika mwezi wa tano mwaka jana ZECO FC
inatarajia kufanya safari ya kimichezo kuelekea Tanzania Bara na kucheza mechi
mbili za kirafiki.
Kikosi
cha timu hiyo kilichoshika nafasi ya kwanza na kutwaa ubingwa kwa taasisi mbali
mbali za Zanzibar katika kilele cha sherehe za mei mosi kinatarajiwa kusafiri
siku ya Alhamis na kupiga ndinga na kuwafundisha ndugu zao wa TANESCO huko
Tanzania Bara siku ya Jumamosi ya tarehe 28/02/2015.
Mechi
hiyo imeandaliwa ikiwa na lengo la kusherehekea ubingwa walioupata kwa kuibuka
kidedea kwa kuzigaragaza taasisi zilizoshiriki mashindano ya mei mosi mwaka
jana, vile vile ziara hiyo ina lengo la kuimarisha udugu na ushirikiano wa
utoaji huduma ya umeme uliopo baina ya ZECO na TANESCO.
Kabla
ya kucheza mechi hiyo na ndugu zao TANESCO, kikosi hicho kinatarajiwa kucheza
mechi ya utangulizi itakayopigwa siku ya Ijumaa ya tarehe 27/02/2015 baina ya
ZECO FC na kikosi cha timu ya Best Point Hotel Limited iliyopo Dar es Salaam.
Timu
hiyo, itaondoka na msafara wa wachezaji pamoja na viongozi wa timu na watendaji
wa Shirika la Umeme Zanzibar (ZECO) na kurejea nyumbani siku ya Jumapili tarehe
mosi, mwezi wa tatu.
No comments:
Post a Comment