DK. HOMERA AIAGIZA THBUB IWE SEHEMU YA ULINZI NA AMANI NCHINI

Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera (katikati) akizungumza na watumishi wa THBUB (hawapo pichani) wakati wa ziara ya kuitembelea ofisi hiyo makao makuu Dodoma, kulia ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Zainabu Katimba na Mwenyekiti wa THBUB, Mhe. Jaji Mathew Mwaimu (Mst) (wa kwanza kushoto). Picha na THBUB.

NA MWASHAMBA JUMA, THBUB

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imetakiwa kuwa sehemu ya kulinda amani ya nchi ili kuipa Tanzania sura nzuri ndani na nje ya mipaka yake.

Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera alipozungumza na Viongozi na watumishi wa tume hiyo wakati wa ziara yake katika ofisi za THBUB Makao Makuu, Jijini Dodoma, Novemba 26, 2025.

Mhe. Homera ameeleza kuwa THBUB imepewa mamlaka makubwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa nakuhifadhiwa nchini Tanzania ili amani iliyokuwepo enzi na enzi iendelee kudumishwa.

“Tumekuwa kimbilo la wengi sababu ya amani tuliyo nayo nchini. Hili ni tunda tunalojivunia, ninyi THBUB ni jukumu lenu kuwaelimisha wananchi kuhusu haki na wajibu pamoja na umuhimu wa kuilinda amani iliyopo" Alieleza Mhe. Homera

Aidha, Mhe. Dkt. Homera ameipongeza THBUB kwa namna inavyotekeleza majukumu yake kwa weledi na kuahidi kutoa ushirikiano katika kipindi chote atakachotumika akiwa Waziri wa Katiba na Sheria kwa maslahi mapana ya Taifa.

Akizungumza katika hafla hiyo wakati akimkaribisha Mhe. Waziri, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainabu Katimba ametoa wito kwa THBUB wakiwa wanatekeleza majukumu yao, kuwakumbusha wananchi kuwa haki na wajibu ni mambo yanayokwenda sambamba na kuwa haki za binadamu zina wigo mpana lakini zina mipaka pia.

“Kila mtu ana wajibu wa kuhakikisha anapo furahia haki zake za msingi haiingilii haki za mwingine” Alisema Mhe. Katimba.

Naye Mwenyekiti wa THBUB, Mhe. Jaji Mathew Mwaimu (Mst) akitoa taarifa ya utekelezaji wa tume hiyo, ameishukuru Wizara ya Katiba na Sheria kwa namna inavyoendelea kushirikiana na Tume kwa kuiwezesha kutekeleza majukumu yake na kuahidi kuendeleza ushirikiano uliopo.

1. Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera (katikati) akizungumza na watumishi wa THBUB wakati wa ziara ya kuitembelea ofisi hiyo makao makuu Dodoma, Novemba 26, 2025.

   Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Zainabu Katimba (kulia)akizungumza na watumishi wa THBUB (hawapo pichani) wakati wa ziara yake na Waziri wa Wizara hiyo kwa THBUB (katikati) wa Kwanza kushoto ni Mwenyekiti wa THBUB, Mhe. Jaji Mathew Mwaimu (Mst).

.    Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Homera (katikati aliyekaa) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa THBUB alipowatembelea Makao Makuu jijini Dodoma, Novemba 26, 2025. Wapili kushoto (aliyekaa) ni Naibu Waziri Mhe. Zainabu Katimba na wapili kulia (aliye kaa) ni Mwenyekiti wa THBUB, Mhe. Jaji Mathew Mwaimu (Mst). Picha na THBUB.

Post a Comment

0 Comments