Na Haji Nassor, Pemba
WAPIGANAJI wa jeshi la Polisi kisiwani Pemba, wametakiwa kuwa mfano mzuri wa
kuziheshimu na kuzitii haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na kuacha tabia ya
kuwachapa makofi na mateke, watuhumiwa wanapowakamata.
Kauli
hiyo imetolewa na Mkuu wa Usalama barabarani Mkoa wa Kusini Pemba, Shawal
Abdalla Ali, alipokuwa akifungua mafunzo ya siku mbili ya haki za binadamu,
yaliowashirikisha askari wa usalama barabarani 40, kutoka mikoa wili ya Pemba.
Alisema
pindi askari akiwa anaziheshimu na kuzitii kwa kina haki za binadamu kuanzia
tokea ukamataji, inaweza kujenga misingi imara na endelevu kwa jamii juu ya
haki hizo.
Mkuu
huyo wa usalama barabarani alieleza kuwa, wapo baadhi ya askari wamekuwa na
mikono mepesi kuwatwanga makofi, mateke na kuwanyima haki nyengine mtuhumiwa,
jambo ambalo kisheria halikubaliki.
“Sisi
askari lazima tuwe mfano mzuri wa kuigwa kwenye eneo hili la kuheshima haki za
binadamu, na ndio jamii itajenga nidhamu miongoni mwao katika hilo na kutuamini’’,alifafanua.
Katika
hatua nyengine Mkuu huyo wa usalama barabarani, alisema askari asiefuata
maadili ya kazi zake na sheria za nchi, huwa ni mbabaishaji na hupelekea
kulivuruga jeshi zima kwenye utendaji.
Mapema
Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba Fatma Khamis
Hemed, wakati akiwasilisha mada ya ufafanuzi wa katiba ya Zanzibar ya mwaka
1984, alisema Katiba hiyo imejenga kwa misingi kadhaa.
Aliyataja
misingi hiyo ni mamlaka kuwa kwa wananchi, katiba kushika hatamu, mgawanyo wa
madaraka, uwakilishi wa wananchi kwenye baraza la wawakilishi, uhuru wa
mahakama pamoja na utawala wa sheria.
Hata
hivyo alisema suala la kuiwelewa katiba na sheria nyengine ni jukumu la kila
mwananchi, sambamba na kujenga mazingira imara ya kuitii.
Nae
Afisa Mipango wa Kituo hicho, Siti Habibu Mohamed akiwasilisha mada ya haki za
binadamu, alisema haki hizo ni za asili ambapo kila mmoja anakuwa nazo.
Alifafanua
haki ya kwanza na ya msingi, ni ya uhai ambapo kama ikiondolewa na nyengine
hukatika kutokana na kuondoa msingi mkuu.
Katika
mafunzo hayo ya siku mbili, mada kadhaa zilijadiliwa ikiwa ni pamoja haki za
binadamu, sheria usalama barabarani, ufafanuzi wa Katiba ya Zanzibar ya mwkaa
1984, ambapo huo ni muendelezo ya mafunzo ya kuwajengea uwezo askari Polisi.
No comments:
Post a Comment