Habari za Punde

PSPF Waanzisha Kampeni ya Mpya ya Mtaa kwa Mtaa.

Balozi wa mfuko wa pensheni wa PSPF Mrisho Mpoto Maalufu kama (Mjomba)  akizungumzana vyombo vya habari kuhusu kampeni ya mtaa kwa mtaa iliyofanyika jijini Dar kushoto ni Afisa wa mfuko wa pensheni wa PSPF Hadji Hamis Jamadary.

Na Mwandishi Wetu
Mfuko wa hifadhi za jamii wa pensheni (PSPF) kwa kuwajali watanzania waanzisha kampeni ya mtaa kwa mtaa ili kuweza kuungana na wananchi wa maeneo mbalimbali kwa kuwapa elimu  inayohusu mfuko huo wa pesheni kampeni hizo zimeanzia jijini Dar es salaam kwa kutembelea wilaya zote tatu huku wakipita mitaa mbalimbali ya wilaya hizo.

Kampeni hiyo imeanza muda mfupi tu mara baada ya mfuko wa pensheni wa PSPF kuungana kwa kutoa huduma na Mfuko wa afya wa NHIF ambapo wanachama wote walio jiunga na kusajiliwa na mfuko wa PSPF watapata manufaa ya kutibiwa kupitia mfuko huo wa afya  wa NHIF kutokana na kuwa wanachama hai.

Balozi wa mfuko wa pensheni wa PSPF Mrisho Mpoto Maalufu kama (Mjomba) pia naye aliweza kuungana na maafisa wa PSPF kwa kwenda kutoa elimu juu ya uchangiaji wa hiari ambao unamuhusu kila mmoja katika jamii zetu Mpoto amesema kuwa kwa kuonesha mfuko wa PSPF hauko mbali na wala haujawatenga wananchi uliamua kuaznisha uchangiaji wa hiari ili kuwapa fursa watanzania na kunufaika na mifuko ya jamii hususani PSPF ambao wanamjali na kuthamini kila mtanzania


Naye kiongozi wa msafara katika kampeni ya mtaa kwa mtaa iliyoanza jijini Dar es salaam Afisa wa mfuko wa pensheni wa PSPF Hadji Hamis Jamadary amesema "Tumeweza kuzunguka katika maeneo mbalimbali ya jiji ndani ya wilaya zote tatu ambazo ni ILALA,KINONDONI na TEMEKE kwa kuwapa elimu wananchi ya namna watakavyo weza kunufaika na mfuko huu wa jamii" ambapo alisema wananchi wamekuwa na mwitikio mkubwa sana hasa kwakuona mfuko wa pensheni wa PSPF umeamua kuwafuata katika maeneo yao na kuwapa elimu hiyo ya uchangiaji wa hiari.

Pia Afisa matekelezo wa mfuko wa pensheni wa PSPF Albert Feruzi amesema katika kuendeleza kutekeleza majukumu waliyo pewa ni pamoja na kuwajuza wananchi kitugani kinacho toka katika mfuko wa PSPF ambapo alisema kwa kila mwananchi atakaye jiunga na kusajiliwa na mfuko ataweza kunufaika na huduma mbalimbali zinazopatikana PSPF pekee na wala sio kwingine alizitaja baaadhi ya huduma ikiwa ni pamoja na kupata mikopo mbalimbali kwa wajasiliamali,mkopo wa nyumba zilizopo katika mikoa mbalimbali ya Tanzania  cha muhimu ni kujiunga na kuwa mwanacha uliye hai ambaye kila wakati unakuwa na uwezo wa kuchangia kila mwezi

Aidha naye afisa uendeshaji wa mfuko wa pensheni wa PSPF Dolphin Richard aliweza kupata fursa ya kuongea na wananchi katika maeneo mbalimbali huku akisisitiza suala la kuwa  ni mmoja wa wanafamilia wa PSPF kutakupa faida nyingi ikiwa ni pamoja na kupata matibabu kwa bima kwakuwa wameweza kuungana na NHIF ilikuleta maendeleo katika taifa la Tanzania
 Pia kunukuu kauli mbiu ya Rais wa Jamuhuri Ya Muungano ya Tanzania Mh.John Pombe Magufuli  akisema (PSPF HAPA KAZI TU) amabapo watahakikisha wanakuwa bega kwa bega na wananchi ili kila mmoja awe na usawa wa maisha naye alitaja baadhi ya mafao wanayo yatoa  ambapo ni fao la kustaafu kazi,fao la elimu,fao la uzazi.
Balozi wa mfuko wa pensheni wa PSPF Mrisho Mpoto Maalufu kama (Mjomba) akitoa burudani pamoja na kutoa elimu kwa wananchi waliofika kupata elimu juu ya Mfuko wa Pensheni wa PSPF hasa katika uchangiaji wa Hiari kupitia kampeni ya mtaa kwa mtaa iliyofanyika jijini Dar
Afisa wa mfuko wa pensheni wa PSPF Hadji Hamis Jamadary akitolea ufafanuzi kuhusu umuhimu wa kujiunga na mfuko wa PSPF hasa katika uchangiaji wa Hiari ambapo aliwasisitiza wananchi kuwa kila mwananchi anaweza kujiunga na mfuko huo na kusisitiza hakuna makato yoyote anayokatwa mteja anapojiunga na mfuko huo.
Wananchi wakendelea kufuatilia kwa makini elimu iliyokuwa ikitolewa na maafisa wa PSPF kupitia kampeini yao ya Mtaa kwa Mtaa.
Afisa wa mfuko wa pensheni wa PSPF Hadji Hamis Jamadary akiwagawia wananchi fomu za kujiunga na uananchama wa mfuko wa PSPF 
 Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Delphin Richard akizungumza na wananchi hawapo pichani wakati wa zoezi ka kuwasajili wananchi kupitia kampeni ya Mtaa kwa Mtaa kuhusu huduma zitolewazo na Mfuko wa Pensheni wa PSPF hasa katika uchangiaji wa hiari ambapo mtu yeyote anaweza kujiunga
Afisa Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Delphin Richard akimpiga picha kwa ajili ya kutengenezewa kitambulisho mmoja wa wanachama waliojiunga na mfuko wa PSPF kupitia kampeni ya Mtaa kwa Mtaa iliyofanyika jijini Dar
Baadhi ya waananchi wakijaza fomu za kujiunga na mfuko wa PSPF  hasa katika uchangiaji wa hiari ambapo mtu yeyote anaweza kujiunga ambapo kila mwananchi anaweza kujiunga.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.