Habari za Punde

Matukio ya uchomwaji moto kisiwani Pemba


 JENGO ambalo lilikuwa kituo cha Afya cha Kiuyu Minunwini, ambalo kwa sasa lilikuwa limehifadhiwa dawa zilizokuwa zimepitwa na muda, vitabu vya skuli ya Minungwini, limeteketea lote kwa moto, usiku wa kuamkia Machi 12 mwaka huu, moto uliosadikiwa kutiwa majira ya saa 10: 00 alfajiri, na kufanya idadi ya matukio hayo kufikia nane Kisiwani Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).



TAWI la Chama Cha Mapinduzi CCM Tibirinzi wilaya ya Chake chake, likiwa limekumbwa na zahma ya kuungua moto, ambapo moto huo umejumuisha matukio nane kisiwani Pemba yalioripotiwa kutokezea usiku wa kuamkia Machi 12 kisiwani humo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.