Na Haji Nassor, Pemba
AFISA Mdhamini wizara ya Nchi Ofisi
ya rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora Pemba Massoud Ali
Mohamed, amewataka wakuu wa Idara zilizomo ndani ya wizara hiyo, kuwaonyesha
haki wafanyakazi wao, na sio kuwakumbusha wajibu wao pekee.
Alisema
moja ya kazi kubwa ya wakuu hao wanapokuwa kwenye vikao vyao, ni kuwaleza
watendaji wao juu ya haki zao, kwa mujibu wa sheria na kanuni za utumishi wa
umma, badala ya kuwasomea na kurejea mara kwa mara wajibu na majukumu yao.
Afisa
Mdhamini huyo, alieleza hayo jana alipokuwa akizungumza na wakuu wa Idara hizo,
kwenye mkutano maalum uliofanyika kwenye ukumbi wa wizara hiyo mjini
Chakechake.
Alieleza
kuwa, ingawa haki kwanza hufuatiwa na wajibu na jukumu la mfanyakazi, lakini
wasisahau kuwaleza haki zao, ili wapate nguvu na moyo kwenye utendaji wao wa
kazi za kuihudumia jamii iliopo.
Aidha
Afisa Mdhamini huyo, alisema suala la kufanya kazi kwa kufuata sheria na
maadilini ya utumishi, ndio njia bora ambayo itawaepusha wafanyakazi, kufanya
kazi zao za kila siku kwa mazoea.
“Jamani
sisi wakuu wa maidara, lazima pamoja na kuwahimiza watendaji wetu kazi, zao
lakini pia tuchukue muda kuwaelimisha na kuwatajia kwa kina juu ya haki zao’’,alifafanua.
Akizungumzia
kuhusu ushirikiano baina ya taasisi moja na nyengine, alisema ndio njia pekee
ambayo itarahisisha kazi zao za kila siku, badala ya kila mmoja kujifungia na
kuendesha shughuli zake.
“Mimi
naamini mahakama, afisi ya mkurugenzi wa mashitaka, afisi ya wakfu, ZAECA
mkifanya kazi kwa kushirikiana, mnaweza kutoa huduma bora na ilio nzuri kwa
wananchi wetu’’,alifafanua.
Kwa
upande wake katibu wa afisi ya Mufti Pemba sheikh Abrhaman Ali Naam, alisema
kutokana na ushirikiano anazo kumbukumbu kwa miaka iliopita kufanikisha vyema
majukumu yao.
Nae
Mwanasheria dhamana wa ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka Pemba Ali Rajab Ali,
alisema suala la kutoa taarifa kutoka Idara moja kwenda nyengine, lazima liwe
na mipaka kutokana na kila Idara kuwa na sheria zake za ndani.
“Mimi
sina wasiwasi juu ya kupashana habari, lakini lazima tusisahau kuheshimu sheria
za utumishi na katiba jinsi ilivyoelekeza namna ya kutunza siri za
ofisi’’,alifafanua.
Katika kikao hicho cha kawaida ambacho kimejumuisha
Idara kadhaa zilimo ndani ya wizara ya nchi, Ofisi ya rais, Katiba, Sheria,
Utumishi, Umma na utawala bora pia kilitumika kwa ajili ya afisa mdhamini huyo
kujitambulisha kwa wakuu wa Idara
No comments:
Post a Comment