Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Dk.Suzan Alphonce Kolimba wakati alipofika Ikulu Mjini Unguja leo,[Picha na Ikulu.] 12/10/2016.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na mgeni wake Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Dk.Suzan Alphonce Kolimba wakati alipofika Ikulu Mjini Unguja leo,[Picha na Ikulu.] 12/10/2016.
STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 12.10.2016
SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kuiimarisha
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa mashirikiano ya
pande zote mbili za Muungano ili iendelee kuleta manufaa na kuzidi kuitangaza
vyema Tanzania Kitaifa na Kimataifa.
Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein aliyasema hayo leo
wakati alipokuwa na mazungumzo na Naibu
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Dk. Susan Alphonce Kolimba aliyefika Ikulu Mjini Zanzibar.
Katika mazungumzo
hayo, Dk. Shein alieleza kuwa Serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweza kujijengea sifa kubwa katika nchi za
Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na hata nje na ndani ya Bara la Afrika
hivyo, kuimarika kwa Wizara hiyo kutaongeza kasi ya kutekeleza majukumu yake
hayo.
Dk. Shein alisema kuwa
mashiriakino ya pamoja ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yameweza kuleta
mafanikio ndani ya Wizara hiyo, hivyo kuna kila sababu ya kuimarishwa zaidi ili
malengo yaliyokusudiwa katika Wizara hiyo yaweze kufikiwa.
Aidha, Dk. Shein
alitumia fursa hiyo kuupongeza uongozi wa Wizara hiyo kwa kazi nzuri inaoendelea kuifanya katika kuhakikisha mafanikio zaidi yanaendelea
kupatikana.
Pamoja na hayo, Dk.
Shein aliupongeza uwamuzi mzuri wa Naibu Waziri huyo wa kufanya ziara katika
Ofisi zake zilizopo hapa Zanzibar kwani atapata fursa nzuri ya kukaa na viongozi
pamoja na watendaji wa Ofisi hiyo na kuzungumza nao masuala mbali mbali ya kazi
zao huku akimsisitiza kuwa ziara hizo ziwe endelevu.
Katika mazungumzo
hayo, Dk. Shein alizipongeza juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Jumuiya ya
Afrika ya Mashariki ikiwa ni pamoja na kuendelea kuithamini Zanzibar na kuishirikisha kikamilifu kwa kutambua
umuhimu wake ndani ya Jumuiya hiyo huku akirejea pongezi zake kwa Bunge la
Jumuiya hiyo kwa kuja kufanya mkutano wake unaoendelea hapa Zanzibar.
Dk. Shein
alimuhakikishia Naibu Waziri huyo kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
itaendelea kutoa ushirikiano wake katika Jumuiya hiyo ili kuhakikisha kuwa inapata
manufaa katika kufikia lengo lililokusudiwa.
Vile Vile, Dk. Shein
aliitumia fursa hiyo kumueleza Naibu Waziri huyo kuwa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar itaendelea kutoa ushirikiano wake katika kuhakikisha Wizara hiyo
inaimarika zaidi ili iweze kuendelea kuwa na sura ya Muungano.
Nae Waziri wa Mambo ya
Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Susan Alphonce Kolimba alimuelezea
Dk. Shein shughuli zinazofanywa na Wizara hiyo pamoja na kueleza kazi
zinazofanywa na Wizara hiyo ndani ya Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki hivi
sasa.
Dk. Kolimba alitumia
fursa hiyo kumpongeza Dk. Shein kwa kuendelea kutoa miongozo na ushauri mzuri ambao
umekuwa chachu katika kuendeleza Wizara hiyo na kumpongeza kwa hotuba yake
nzuri aliyoitoa hapo jana katika Mkutano
wa Pili wa Kikao cha Tano cha Bunge la Tatu la Jumuiya ya Afrika Mashariki..
Aidha, Dk. Kolimba
alimuhakikishia Dk. Shein kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki itaendelea kutoa fursa
sawa kwa pande zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kusisitiza
mashirikiano yanaimarishwa katika kuiongoza Wizara inayoshughulikia Mambo ya
Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Pamoja na hayo, Dk.
Kolimba alipongeza juhudi za makususdi zinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar chini ya uongozi wa Dk. Shein katika kuwaletea maendeleo wananchi
wake wote.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment