Habari za Punde

Mkutano kuwajengea uelewa viongozi kuhusu mpango wa kunusuru kaya masikini Pemba

 MAAFISA Wadhamini Kutoka taasisi mbali mbali za Serikali Kisiwani Pemba, wakifuatilia hutuba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe:Mohamed Aboud Mohamed, wakati alipokuwa akifungua Mkutano huo huko nje kidogo ya Mji wa Chake Chake Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA)
WAKUU wa Wilaya kutoka Wilaya nne za Micheweni, Chake Chake, Mkoani na Wete Kisiwani Pemba, wakifuatia kwa makini hutuba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe;Mohamed Aboud Mohamed, hayupo pichani wakati akifungua kikao cha kuwajengea uelewa viongozi kuhusiana na mpango wa kunusuru kaya masikini Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA)

  AFISA Mdhamini Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Pemba, Salum Ali Matta, akiwakaribisha wageni katika mkutano kuwajengea uelewa viongozi kuhusu mpango wa kunusuru kaya masikini Pemba, mkutano huo uliofanyika nje kidogo ya mji wa Chake Chake.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA)

 MKURUGENZI Mtendaji wa TASAF Makao Mkuu, Ledislaus Mwamanga akitoa maelezo ya jumla juu ya mpango wa kunusuru kaya masini Tanzania, katika mkutano uliowashirikisha viongozi mbali mbali uliofanyika Wesha nje kidogo na mji wa Chake Chake.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA)
 NAIBU Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Ahmad Kassim Haji, akizungumza katika mkutano uliowashirikisha Viongozi mbali mbali wa Serikali, juu ya mpango wa kunusuru kaya masikini Pemba, uliofanyika nje kidogo ya mji wa Chake Chake Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA)
 MWENYEKITI wa Kamati tekelezaji ya Tasaf Pemba, ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba Mhe;Mwanajuma Majid Abdalla, akizungumza neno katika mkutano wa kuwajengea uwelewa Viongozi juu ya mpanbgo wa kunusuru kaya masikini Pemba, uliofanyika nje kidogo ya Mji wa Chake Chake Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA)

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe:Mohamed Aboud Mohamed akifungua mkutano maalumu wa kuwajengea uelewa viongozi wa Serikali juu ya Mpango wa kunusuru kaya masikini Pemba, uliofanyika nje kidogo wa mji wa Chake Chake.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA)

MKUU wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Omar Khamis Othaman, akitoa neno la shukurani baada Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe:Mohammed Aboud Mohammed, kufungua mkutano maalumu wa kuwajengea uwelewa Viongozi wa Serikali juu ya Mpango wa Kunusuru kaya masikini Zanzibar.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA)
VIONGOZI mbali mbali wa Serikali wakiongozwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe:Mohammed Aboud Mohammed, katikati wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kufungua mkutano maalumu huko Wesha nje kidogo ya mji wa Chake Chake.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.