STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 10.1.2017

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein ameipongeza Jamhuri ya Korea kupitia Mashirika yake kwa kuendelea
kuiunga mkono Zanzibar katika sekta za maendeleo ikiwemo sekta ya elimu.
Dk. Shein aliyasema
hayo kwa nyakati tofauti alipokutana na uongozi wa Shirika la Maendeleo la
Kimataifa (KOICA) ukiongozwa na Makamu wa Rais wa KOICA pamoja na kufanya
mazungumzo na uongozi wa Seoul Broadcasting System (SBS TV), Ikulu mjini
Zanzibar.
Katika mazungumzo
hayo, Dk. Shein alisema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inathamini
juhudi hizo za Mashirika hayo ya Korea katika kuunga mkono harakati za
maendeleo hapa Zanzibar na kueleza kuwa mradi wa skuli ya Kwarara ni wa mwazo
katika miradi ya elimu ambayo haijawahi kutokea.
Dk. Shein alisema kuwa
Tanzania na Jamhuri ya Korea zilianza mahusiano ya Kidiplomasia mnamo mwaka
1999 ambapo nchi hiyo imeweza kuisaidia Tanzania ikiwemo Zanzibar mambo mbali
mbali ikiwemo sekta ya elimu, kuimarisha kilimo cha mpunga, kilimo cha
umwagiliaji maji na hivi karibuni mradi wa kufuga samaki nao unatarajiwa kuanza.
Katika mradi huo mpya
wa kufuga samaki Dk. Sgein alisema kuwa umradi huo utazalisha vifaranga vya
samaki na majongoo ya bahari huko Beit-el-Rais mradi ambao utagharamiwa na
KOICA.
Dk. Shein alitumia
fursa hiyo kutoa pongezi kwa Korea kupitia mashirika yake hayo kwa ujenzi wa
skuli mpya ya kisasa na ya aina yake huko Kwarara inayotarajiwa kufunguliwa
kesho (11.1.2016) ambapo alisema hiyo ni ishara ya urafiki kati ya nchin hiyo
na Zanzibar.
Nao uongozi wa KOICA
umetoa pongezi kwa Dk. Shein kwa mafanikio makubwa yaliofikiwa hapa Zanzibar na
kuahidi kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika kuimarisha sekta za maendeleo
ikiwemo sekta ya elimu.
Shirika la SBS
lilieleza kuwa mikakati yao ni kujenga skuli mia moja katika bara la Afrika na
skuli hiyo ya Kwarara ni ya Miamoja kati ya 99 ambazo wamejenga katika nchi
nyengine ila kwa upande wa skuli hiyo ni ya kipekee kutokana na kuwa na studio
na mambo mengine ya habari, mradi ambao KOICA nao wamesaidia kwa asilimia 50.
Sambamba na hayo,
Shirika la KOICA linatarajia kutoa msaada wa dola za Kimarekani milioni 10
ambazo zitapitia kwa Shirika lisilo la Kiserikali la Korea kwa ajili ya
kuimarisha elimu ya Sekondari kwa wanafunzi wa kike.
Aidha, Shirika la Good
Neighbors Tanzania wamekubali kujenga skuli ya msingi huko Kwarara itakayokuwa
na madarasa 24 ambapo tayari eneo la skuli hiyo limeshapatikana.
Pamoja na hayo, KOICA
imeahidi kuunga mkono katika miradi mengine mipya itakayoianzisha hapa Zanzibar
huku wakitumia fursa hiyo kutoa shukurani kwa mashirikiano mazuri waliyayapata
kutoka kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali.
Shirika la SBS TV
limeadihi kuitangaza Zanzibar nchini mwao sambamba na kuutangaza utamaduni wa
Zanzibar kutokana na vipindi maalum vya Televisheni watakavyovitengeneza ambapo
pia uongozi huo ulimpongeza Dk. Shein kwa juhudi zake za kuchapa kazi .
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment