Kushoto aliekua
mratibu wa elimu masafa Pemba Malim Haji Hamad Hassan (Mstaafu), katikati ni
Mratibu wa Idara ya Mafunzo ya ualimu Pemba na kulia ni Malim Faki Sleyyum Faki
Maalim Haji Hamad Hassan akiwa na zawadi ambayo alikabidhiwa na Malim Mkubwa Ahmed Omar kwa niaba ya wafanya kazi wa idara ya mafunzo ya Ualimu Kisiwani Pemba
Na Ali Othman, Pemba
Mratibu wa Idara ya mafunzo ya ualimu Pemba Malim Mkubwa Ahmed Omar amewataka watendaji katika idara yake kuiga mfano wa aliekua mratibu wa mafunzo ya elimu masafa Pemba Maalim Haji Hamad Hassan ambae amestaafu rasmi hivi karibuni.
Akizungumza katika hafla fupi ya
kumuaga aliekua Mratibu wa elimu masafa Pemba, Malim Mkubwa amempongeza kwa
kufikia umri wa kustaafu akiwa na heshima kubwa kutokana na juhudi zake katika
kusimamia majukumu yake. Amewaomba watendaji wengine katika idara hiyo kuiga
mfano huo kwa kutekeleza majukumu yao ya kila siku kwa bidii na juhudi kubwa.
Akitoa takwimu za wahitimu wa elimu
masafa ambao walihitimu katika kipindi chake akiwa mratibu wa elimu masafa
Pemba, Malim Haji amesema jumla ya wahitimu 805 wamehitimu mafunzo ya ualimu na
kupatiwa vyeti kupitia elimu masafa kisiwani Pemba.
Wakati huo huo Mratimu wa mafunzo ya
Ualimu kisiwani Pemba Malim Mkubwa Ahmed Omar amemkabidhi Mstaafu huyo zawadi
ya Cherahani ambayo amezawadiwa na watendaji wa idara vikiwemo vituo vya walimu
kisiwani Pemba.
Ametoa historia yake nakusema
kwamba, juhudi zake katika kazi zilianza tokea mwaka 1975 ambapo alianza kazi
akiwa mwalimu katika skuli ya Kangagani. Ameongeza kwamba alitumikia nafasi
hiyo ya kuelimisha hadi mwaka 2001 ambapo alipata nafasi ya Uratibu wa elimu
masafa Pemba nafasi ambayo kwasasa inashikiliwa na Malim Hemed Said Masoud
baada ya kustaafu kwake.
No comments:
Post a Comment