Na.Haji Nassor. Pemba.
KATIBU Tawala mpya wa wilaya ya
Mkoani Pemba, Miza Hassan Faki, amewaomba viongozi wa wilaya hiyo, pamoja na
mkoa wa kusini Pemba, kumpa kila aina ya ushirikiano, ili atimize majukumu yake,
kwenye nafasi hiyo.
Alisema,
kama viongozi wenzake hawakumpa ushirikiano, kumkosoa, kumuelekeza na
kumuonyesha njia za kutekeleza majuku yake, kamwe lengo la kuwahudumia wananchi
wa wilaya hiyo hatolifikia.
Katibu tawala wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki,
akila kiapo cha kushika nafasi hiyo.
Katibu
Tawala huyo, alieleza hayo ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba,
muda mfupi mara baada ya Mkuu wa mkoa huo Mwanajuma Majid Abdallah, kumuapisha
kushika majukumu yake, kufuatia uteuzi wake uliofanya na rais wa Zanzibar Juni
19 mwaka huu.
Alisema,
yeye ni mdogo kiumri, elimu na anaouzefu mdogo kwenye uongozi, hivyo kwa kiasi
kikubwa anawategemea viongozi hao, ili afanikishe vyema utekelezaji wa Ilani ya
CCM ya mwaka 2015/2020 kwenye nafasi yake hiyo.
“Mimi bado
mdogo kwenye uongozi jamani, sasa lazima mnishauri, mnielekeze, mniambie na
muniite mkiona naenda kombo, mkifanya hivyo lengo la Rais kuniteua
litafikiwa”,alisema.
Mapema Mkuu
wa Mkoa huo, Mwanajuma Majid Abdalla, alisema rais hakukosea kumteua Katibu
tawala huyo, kutokana na umahiri wake kwenye kazi.
Alisema, kwa
vile anamfahamu vyema Katibu tawala huyo, anaamini hakutakuwa na kazi kubwa ya
kumuelekeza kwenye nafasi yake hiyo mpya.
“Mimi
naamini, mkuu wa wilaya ya Mkoani Hemed Suleiman Abdalla, hatokuwa na kazi
kubwa sana kwa Katibu tawala wake, maana anaweza na anafundishika”,alieleza.
Kwa upande
wake, Katib Tawala Mkoa wa Kusuini Pemba Yussuf Mohamed Ali, alimtaka Katibu
tawala huyo wa wilaya ya Mkoani, kubisha hodi kila mara kwenye ofisi yake,
ikiwa atahitaji maelekezo.
Mkuu wa
wilaya ya Mkoani Hemed Suleiman Abdalla, alimueleza Katib tawala huyo, kukubali
kufundishwa, kuelekezwa na kukosolewa, ikiwa ni njia moja wapo ya kuelekea
mafanikio.
Aidha Hemed,
alimueleza Katibu huyo, kwa vile anaongoza jamii kubwa ya watu, ajue kuwa,
atakumbana na vikwazo, makero, shida, watu kutomkufahamu ingawa yote hayo ni
sehemu ya uongozi.
Rais wa
Zanzibar na Mwneyekiti wa baraza la Mapinduzi Zanzibar Mhe: dk Ali Mohamed
Shein, kwa kutumia kifungu cha 15 (1,2,na 3) sheria no 8 ya mwaka 2014 ya
Tawala za Mikoa alifanya utezi wa viongozi mbali mbali, akiwemo Katibu tawala
wilaya ya Mkoani Miza Hassan Faki.
No comments:
Post a Comment