Habari za Punde

Wakulima jimbo la Ukele Micheweni kukosa kuvuna zao la mpunga

Na Salmin Juma, Pemba


Zaidi ya wakulima 300 katika bonde la Ukele Wilaya ya Micheweni huenda wakakosa kuvuna zao la mpunga baada ya mashamba yao kuingia majichumvi yaliyochanganyika na maji ya mvua zinazoendelea kunyesha na kusababisha kuvunja tuta na kuingia katika mashamba hayo.

Baadhi ya wakulima hao wamesema awali walikuwa na matumaini ya kuvuna lakini baada ya kuingia maji chumvi imesababisha kilimo hicho kuungua

Akizungumza na wakulima hao Naibu waziri wa nchi ofisi ya makamo wa pili wa rais Mh Mihayo Juma Mhnunga amesema Serikali tayari wameshaiona athari hiyo na hivi sasa wanatafuta njia ya kuliboresha tuta hilo ili wakulima wasiathirike zaidi 

Ameshauri kuwekwa mlango wa dharura wa kusaidia kutoa maji hayo katika mashamba na kurejesha udongo uliochukuliwa na maji ili wale waliokuwa hawajafikwa na maafa hayo wapate fursa ya kuvuna mpunga wao.

Wakati huo huo Mh Mihayo ametembelea barabara ya Gando eneo la Mangwena lililokatika wa mvua na kuwapongeza wafanyakazi kwa kurejesha huduma ya usafiri kwa haraka licha ya uhaba wa vifaa walivyonavyo.


Aidha Naibu waziri huyo ameshuhudia ugawaji wa misaada ya chakula na nguo kwa wananchi waliopatwa na maafa katika majimbo ya Kojani na Micheweni na kuwataka kuwa na umoja na mashirikiano pale wanapokutwa na maafa .

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.