Na.Haji Nassor. Pemba.
Mwalimu Mkuu na waalimu wengine wa
skuli ya Tumbe sekondari wilaya ya Micheweni Kisiwani, umeshindwa kuamini macho
yao hapo juzi, baada ya mzazi Salama Khamis Hamad (65) kutinga skulini hapo
kufuatilia iwapo wajukuu wake wamehdhuria masomo.
Waalimu hao
wakiwa katika maonyesho ya maktaba yalioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria
Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, ghafla mzazi huyo alifika mlangoni mwa darasa
lililokuwa na maonyesho hayo, na kuwauliza wajukuu wake.
Mama huyo
ambaea aliwaacha midomo wazi ya waalimu na wageni wengine kwa ukakamavua na
ujasiri wake, yeye kubwa alitaka kuonyeshwa wajukuu wake wawili iwapo wamefika
skulini hapo.
Mwandishi
wetu aliekuwepo skulini hapo, alielezwa na mama huyo kuwa, amekuwa akipokea
taarifa kwa baadhi ya wanafunzi, kuwa wajukuu wake wamekuwa wakiishia vichakani
na hawaingii darasani.
Alisema
alichokifuata skuli hapo sio jengine bali ni kutaka kujua iwapo wajukuu wake
wako darasani na wanaendelea na masomo.
“Mimi
nilichokifuata skuli ni kutaka kujiridhisha iwapo wajukuu wangu wapo, maana
mimi nahangaika kwa wao mchana mzima, sasa kama hawapo nijuwe vya kufanya”,alisema.
Mlezi huyo
mwenye wajukuu wanaosoma dara la kumi na la tisa skulini hapo, alisema yeye hakubali
kuona wajukuu wake, wanapuuza masomo kwa vile anajua kuwa aliesoma na mwengine
ni tofauti yao.
Katika hatua
nyengine mzazi huyo, alisema wakati umefika kwa wazazi wenzake, kutowatwika
mzigo wa waalimu peke yao, lazima na wao
wawe bega kwa bega katika kumtafutia maendeleo ya mtoto.
“Huyu mtoto
akishasoma na kupata kazi, hata mwalimu wake hamjui tena, sasa lazima sisi
wazazi tuwahimize na kuwafuatilia watoto, maana ni wajanja na
wakorofi”,alifafanua.
Kwa upande
wake Mwalimu Mkuu wa skuli hiyo, Nassor Bakar Said, alisema ujasiri wa mlezi
huyo pamoja na umri wake, umewatia moyo sana katika kazi zao.
Mwalimu mkuu
huyo, alisema inawezekana mikutano walioifanya hivi karibuni ya kuwataka wazazi
wafuatilie masomo ya watoto wao yameanza kuzaa matunda.
“Hivi
karibuni tulifanya mikutano katika kijiji cha Raha kesho shehia ya Tumbe, sasa
wazazi pengine wameanza kufuatilia mahudhurio ya watoto wao, sisi twamshukuru”,alifafanua.
Hata hivyo
Mwalimu mkuu huyo, aliwataka wazazi wengine kuiga mfano wa mzazi huyo, maana
waalimu hawana muda wa kuwafuatilia watoto vichakani.
Baadhi ya
wadau wa elimu wa kijiji cha Tumbe, walisema mafanikio ya wanafunzi yanahitaji
nguzo tatu, akiwemo mazizi, mwalimu namwafunzi mwenyewe.
“Mimi kwa
kweli hadi sasa siamini, kuwa umri alionao yule bibi, lakini kuacha kazi zake
na kufika skuli na kufautilia maendeleo ya wajukuu zake, ni mfano hai na
mzuri”,alisema Hamad Faki Hamad.
Nae Afisa
Mipango wa Kituo cha Huduma za Sheria ZanzibarZLSC tawi la Pemba, Siti Habib
Mohamed, alisema amevutiwa sana na umahiri na umakini wa mzazi huyo.
“Mimi
sijawahi kuona wala kusikia mzazi anaefuatilia maendeleo ya watoto wake skuli,
maana hata ukimuona mzazi basi ujue skuli kuna kikao au kaitwa kwa matatizo ya
mtoto wake, lakini kwa huyu kafanya jambo jema na la kuigwa”,alisema.Hata hivyo
badhi ya wanafunzi wa skuli hiyo, walisema ni kweli wapo baadhi yao huaga
nyumbani kwamba wanakwenda skuli, ingawa matokeo yake huishia kwenye vichaka.
No comments:
Post a Comment