Kikosi cha timu ya Gulioni iliyoibuka kifua mbele kwa kuilaza Ujamaa 3-1
Kikosi cha Timu ya Ujamaa iliyolala mbele ya Gulioni
Na: Abubakar Khatib Kisandu, Zanzibar.
Timu kongwe Visiwani Zanzibar Ujamaa Sports Club
wamekubali kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa vijana wa
Gulion FC kwenye mchezo maalum wa Sherehe za kutimiza
miaka 60 kwa Ujamaa mchezo ambao umesukumwa jana
saa 2 za usiku kwenye uwanja wa Amaan.
wamekubali kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa vijana wa
Gulion FC kwenye mchezo maalum wa Sherehe za kutimiza
miaka 60 kwa Ujamaa mchezo ambao umesukumwa jana
saa 2 za usiku kwenye uwanja wa Amaan.
Mabao ya Gulioni katika mchezo huo yamefungwa na Abdul Hamid Ramadhan dakika ya 45, Ali Juma dakika ya 71 na Shaabani Hassan dakika ya 88 huku bao pekee la Ujamaa likifungwa na Mwinyi Ame dakika ya 79.
Ujamaa ndio timu aliyewahi kucheza kwa kiwango cha hali ya juu Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein ambapo Katika mchezo huo Mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Habari Utalii Utamaduni na Michezo Zanzibar Mh Rashid Ali Juma akimuwakilisha Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ambae pia alikuwa mlinda mlango hatari wa timu hiyo miaka iliyopita.
Msimu huu mpya wa mwaka 2017-2018 Ujamaa itashiriki ligi daraja la Pili Taifa Unguja wakati Gulioni FC itacheza ligi daraja la Pili Wilaya ya Mjini.
No comments:
Post a Comment