NA HAJI NASSOR, PEMBA
WAKULIMA na wananchi waliokodia
mashamba ya mikarafuu kisiwani Pemba, wamesema kutokana na msimu wa mwaka huu
kuwa wa aina yake kutokana na mzao kunongoka, wanamatumaini makubwa ya kufanikisha
malengo yao ya kimaendeleo.
Walisema
wanatarajia kukuza na kuendelea biashara zao, mara baada ya kumalizika kwa
msimu wa mwaka huu wa uvunaji na uuzaji wa zao hilo la taifa.
Wakizungumza
na mwandishi wa habari kwa nyakati tofauti, walisema kwa vile msimu ni mkubwa
kuwahi kutokea kama miaka kumi (10) sasa iwapo bei ya shilingi 14,000
itaendelea wanatarajia kupata mafanakio mazuri.
Mmoja
kati ya wakuli hao mkaazi wa Toroni wilaya ya Mkoani Mwantatu Zubeir Mjaka,
alisema karibu misimu mitatu alikuwa hajawi kufunga biashara zake mjini Unguja,
ingawa mwa msimu huu unavyotarajiwa kuwa mkubwa amelezimika kufunga.
“Mimi
namiliki mikarafuu 73 ambayo kwa mzao ulivyo basi kila mkarafuu ntapata pishi
100 mbichi, wastani wa guni moja kavu sasa ntakunja hadi shilingi milioni 1
(1,000,000), sasa hapo piga kwa mikarafuu 73”,alieleza.
Nae
Jabir Idrissa Makame wa Mizingani alisema, pamoja na kumilika mashamba mawili
inayojumuiasha mikarafuu 400, alisema kwanza anachoomba kwa serikali
kuhakikisha hawashushi bei wala wakulima kukopwa wanapokwenda kuuza ZSCT.
“Mimi
mara nyingi ukimaliza msimu wa uchumaji hupeda kununua aradhi, kama
nilivyofanya mwaka juzi kununua na kupanda miche 100, na mara hii ntafanya
hivyo lakini pia na kunu gari aina ya ‘carry’ kwa ajili ya shughuli
zangu”,alifafanua.
Hata
hivyo mkulima Mmanga Hemed Sultan alienunua shamba la mikarafuu 550 hivi
karibuni mabonde ya Ngomeni na Mgelema alisema anachokusudia kufanya kwa msimu
huu baada ya kutoa haki za watu ni kununua gari moja kwa ajili ya biashara.
“Matumaini
yangu kwanza mpaka nishewalipa vibarua, kutoa gharama za usafishaji wa shamba
lakini baada ya hapo ni kutafuta gari moja aina ya ‘haice’ kwa ajili ya
biashara”,alieleza.
Kwa
upande wake mchumaji maarufu wa karafuu Kassim Haji Kassim (45) wa Ziwani
wilaya ya Chakechake anasema, anachosubiri kwa hamu kwanza ni kuanza kwa msimu,
ambapo malengi yake hapo kisha yatajipanga.
“Mimi
msimu uliopita nilianza ujenzi wa nyumba ya kudumu, na kwa hatua iliobakia kama
matajiri wataniita kuchuma kibarua basi ni kuhakikisha nakamilisha ujenzi kwa
hatua ya kuezeka”,alisema.
Fatma
Muhunzi Ameir (30) wa Piki wilaya ya Wete alieleza kuwa yeye msimu huu itakuwa
ni mara yake ya kwanza kuchuma karafuu, kwa vile alikuwa misimu kadhaa hakuwepo
kisiwa Pemba.
“Mwaka
jana nilimaliza chuo na sasa nipo mtaani, hivyo karafuu zikianza tu name
ntafuata walionayo ili kuchuma, lakini nikipata fedha nataka ninunue cherehani
ya sinja, na kompyuta kwa ajili mwanangu kufanya mazoezi anaporudi
skuli”,alifafanua.
Mdhamini wa Shirika la taifa la ZSTC Kisiwani
Pemba Abdalla Ali Ussi, alisema shirika halina nia wala mpango wa kushusha bei
ya karafuu na waka hakutakuwa na mkulima atakaekopwa fedha wakati anapokwenda
kuuza karafuu zake.
Alisema
Serikali kupitia shirika lake pekee lililoruhusiwa kununua karafuu limejipanga
kuhakikisha linawafikia wananchi na wakulima wote kwenye vituo rasmi vya kuuzia
karafuu, na wala wasikubali kuwauzia watu wengine wanaopita mitaani.
Ussi
hakuwa tayari kutaja kima halisi wanachotarajia kununua kwa msimu huu mpya,
ingawa alisema baadae wataweka bayana, huku akiwasisitiza wananchi kuwa walinzi
wa magendo ya karafauu hizo, ili ziendelea kubakia nchini kwa maslahi ya
wananchi wenyewe.
Msimu
mpya wa uvunaji wa zao la karafuu ambao unatabiriwa kuwa mkubwa kuliko misimu
mengine ya miaka 10 iliopita, umeshazinduliwa na Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar Mhe: Baloz Seif Ali Idd hivi karibuni kisiwani Pemba.
No comments:
Post a Comment