Habari za Punde

Waziri wa Afya awaasa mabinti : msikubali kushikwa shikwa ndio chanzo cha ubakaji


NA HAJI NASSOR, PEMBA

WAZIRI wa Afya Zanzibar Mhe: Mahamoud Thabiti Kombo, amewataka watoto wa kike wa Wilaya ya Micheweni Mkoa wa kaskazini Pemba, wawaripoti watu watakaonza kuwashika shika sehemu zisizostahiki au kuwahonga kwa vizawadi, kwani huo ndio mwanzo wa wao kubwaka hapo baadae.

Waziri Mahamaoud alisema, wapo baadhi ya watu wasiowapendelea maendeleo yao, huanza kuwatambazia mikono kifuani au kuwapa peremendi “pipi” hivyo wanapoona hali hiyo, wasingojee ushahidi kamili na ni vyema wakaripoti katika maeneo husika.

Akizungumza katika ufunguzi wa Kituo cha Mkono kwa Mkono “one stop center” kilichopo hospitali ya Micheweni Mkoani humo, alisema ubakaji huanza na mambo kadhaa yakiwemo hayo aliyoyataja.

Alisema wanafunzi na hasa wakike, wasikubali kusubiri ushahidi kamili kwa vile pana Kituo hicho, bali wajenge utamaduni wa kutoa taarifa kila wanapofanyiwa matendo yasiowaridhisha.

Waziri huyo wa Afya, alisema ingawa Kituo hicho kipo, ingawa hawatarajii kuona matendo ya udhalilishaji ukiwemo ubakaji unaongezeka, bali ni kupunguza na miongoni mwa njia hizo, ni kutoa taarifa pale wanapoonza kushikwa kifua au kupewa pipi.

“Msikubali kuchezewa chezewa, au kushikwa shikwa titi zenu au kupewa vipipi na watu mbali mbali, maana hiyo ndio sababu ya nyinyi wanafunzi na watoto wa kike kubwa”,alifafanua.

Katika hatua nyengine Waziri huyo wa Afya Zanzibar Mhe: Mahamoud Thabiti Kombo, aliwataka wananchi wa Micheweni kushirikiana kwa karibu na watendaji wa Kituo hicho, ikiwa ni njia moja wapo ya kupunguza matendo ya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto.

Hata hivyo alisema watendaji wa Kituo hicho pamoja na madaktari wengine, watajengewa uwezo kwa kupatiwa mafunzo, muda mfupi ujao ili waweze kuwahudumiwa wananchi kwa ufanisi, kama ilivyo amza ya sirikaki kuu.

Kwa upande wake Mratibu Mkuu wa masuala ya ulinzi wa uhifadhi wa mtoto kutoka Shirika la Save Children Zanzibar, Ramadhan Mohamed Rashid, alisema mpango wa kuanzisha vituo vya aina hiyo, ni mpango maalum wa kuunga mkono juhudi za serikali kuu.

Alisema, baada ya wadau mbali mbali wakiwemo na serikali na wizara zake husika, kuona matendo ya udhalilishaji yanaogezeka siku hadi siku, ndio wakabuni na kuanzisha vituo hivyo, ili waathirika wahudumiwe.

Hata hivyo Mratibu huyo, aliwataka madaktari kuacha woga pale wanapotakiwa kufika mbele ya mahakama kutoa ushahidi wao kwa wale watoto waliowahudumia baada ya kubakwa, kunajisiwa au kubebeshwa ujauzito.

Akisoma risala ya wananchi wa Micheweni, daktari wa Hospitali ya wilaya hiyo, Mgeni Haroun Salim, alisema tokea kuanza kwa huduma za mkono kwa mkono wilayani humo mwaka 2014, watoto 14 wameshabakwa, nane ujauzito na watoto 12 waliripotiwa kutoroshwa.

Hata hivyo alisema ujio wa Kituo hicho kipya, sasa kitasaidia kuwafikia wananchi waliowengi, kwanza kuwahamasisha kukitumia Kituo hicho sambamba na kuwaleleza athri za matendo hayo ndani ya jamii.

Nae Mratibu wa Kituo hicho cha Mkono kwa Mkono wilaya ya Micheweni Asma Mohamed Fasihi, akimpa maelezo Waziri wa Afya mara baada ya kukifungua, alisema kilichopo mbele yao sasa ni kuwaelimisha wananchi vijijini.


Kituo cha Mkono kwa mkono kilichomo hospitali ya Micheweni Pemba, ni cha kwanza kati ya vituo vitano vyengine, vinavyotazamiwa kujengwa na Shirika la Save the children, ambapo kwa kisiwani Pemba vipo vituo kama hivyo kwa hospitali za Wete na Chakechake.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.