NA HAJI NASSOR, PEMBA
BODI ya Mapato Zanzibar ZRB, imesema
iko katika hatua za mwisho za kukamilisha utaratibu wa kielektroniki kupitia
simu ya mkononi, ili kuwawezesha wanaopaswa kulipa kodi, kufanya hivyo kwa kupitia
mfumo huo, ambapo utawapunguzia muda wa kuweka foleni kwenye mabenki.
ZRB
imesema, mifumo ya kisasa ya ulipaji wa kodi ukiwemo ule wa kulipitia benki
haitoondolewa, ingawa mlipa kodi atakuwa na njia nyingi zaidi za kulipa madeni
yake, kwa mujibu wa urahisi wake.
Kauli
hiyo imetolewa hivi karibuni na Afisa Mdhamini Elimu kwa walipa kodi kutoka
Bodi hiyo Shaaban Yahya Ramadhan, alipokuwa akizungumza na wafanyabiashara wa
wilaya ya Chakechake, kwenye semini juu ya kueleweshwa mabadiliko ya sheria za
kodi.
Alisema
ZRB imejiandaa vyema kuhakikisha inawarahisishia ulipaji wa kodi wadau wake,
ndio maana imeshaandaa njia ya kupitia simu ya mkononi, ambapo zoezi rasmi
litazinduliwa wakati wowote.
Aidha
alieleza kuwa, kwa sasa wanaendelea na majaribio hayo kwa watendaji wake, na
baadhi ya wafanyabiashara kuanza kuutumia, lakini rasmi muamala huo
utazinduliwa hapo baadae.
“Sasa
mnaotaka kulipa kodia pamoja na zile njia za zamazni lakini, kwa sasa pia tuna
njia nyengine kupitia mtandao wa simu, tembeleeni ofisi zetu mtape maelekezo ya
kina”,alifafanua.
Hata
hivyo Afisa huyo, amewataka wafanyabiashara hao, kujitayarisha kisaikoloji ujio
wa mashine za kielektroniki za utoaji wa risiti, EFD ikiwa ni pamoja na
kujifunza matumizi yake mapema.
Alifahamisha
kuwa faidi ya kubwa ya mashine hizo, hazipotezi mapato, maana zipo kampuni
kabla ya kutumia mashine hizo walikuwa wakilipa kodi shilingi 13 milioni kwa
mwaka, ingawa baada ya kuingia kwenye muamala wao sasa, wanalipwa shilingi
milioni 167.
Kwa
upande wake Meneja Sera, Utafiti, na Mipango kutoka ZRB Zanzibar Ahmed Saadat,
alisema Bodi hiyo, itaendelea kuwaelimsha walipa kodi ili walipe kodi zao kwa
hiari na wala sio kutumia nguvu.
Alisema
ulipaji wa kodi duniani umekuwa na faida kubwa, ikiwa ni pamoja na kuihakikishia
serikali kupanga mikakati yake, ya kimaendeleo kwa jamii.
Baadhi
ya wafanyabiashara wa Wilaya ya Chakechake, wameiomba ZRB kukaa pamoja na TRA
ili kuwe na mkusanyaji mmoja wa kodi ili kuondoa mkanganyiko wakati wa
ukusanyaji.
Khamis
Mohamed Haji, alisema uwepo wa mamlaka mbili zinazokusanya kodi kwa
mfanyabiashara mmoja, ni changamoto ambayo lazima itafutiwe ufumbuzi.
“Sisi
wafanyabishara tunapenda sana kulipa kodi, lakini sio kwa utaratibu huu ualipo,
kuwa kuna TRA, ZRB, mbali mabaraza ya miji na hapo hujangaalia fedha za kodi,
laima ufumbuzi wa kuwa na mkusanyaji mmoja uangaliwe”,alishauri.
Nae
Rashidi Nassor Mohamed “manyimbo” alisema lazima maofisa wanaohusika na
ukusanyaji wa kodi, wawe na lughua nzuri kwao, ili kujenga urafiki wa kikazi.
Katika
semina hiyo ya siku moja, ufafnuzi wa sheria kadhaa
zilijadiliwa ikiwa ni
pamoja na sheria ya ushuru wa stemp na sheria za nyaraka, ambapo tayari
wafanyabishara kadhaa wameshafikiwa na taaluma hiyo.
No comments:
Post a Comment