Habari za Punde

TAMWA Watowa Mafunzo Kwa Wanakamati wa Mradi wa GAWE III Kisiwani Pemba.

MWENYEKITI wa Kamati ya GEWE III, Sheha wa shehia ya Mjini Ole, Khamis Shaaban (katikati), akifungua mkutano wa kuwaelimishwa wanakamati hiyo, aina za kesi za udhalilishaji, mkutano uliofanyika uwanja wa Gombani Chakechake Pemba
MRATIBU wa miradi kutoka TAMWA Asha Abdi Makame, akielezea ujio wa mradi wa kupinga udhalilishaji GEWE III, kwa ajili ya shehia sita za Wiaya ya Wete kisiwani Pemba, mkutano huo ulifanyika uwanja wa Gombani
MWANASHERIA wa serikali kutoka Afisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka Pemba, Mohamed Ali Juma akitoa mada ya aina ya makosa ya udhalilishaji, mbele ya kamati ya mradi wa kupinga  udhalilishaji kupitia GEWE III, uliofanyika uwanja wa Gombani
AFISA Ustawi wa Jamii wilaya ya Wete Haroub Suleiman Hemed, akichangia jambo, kwenye mkutano uliojadili aina ya makosa ya udhalilishaji, kupitia mradi wa kupinga udhalilishaji GEWE III, na kufanyika uwanja wa Gombani Chakechake Pemba
Mwanakamati wa Mradi wa GEWE III, akichangia wakati wa mkutano huo wa siku moja, uliozungumzia aina ya makosa ya udhalilishaji, uliofanyika uwanja wa Gombani Chakechake Pemba, ambapo mradi huo uko kwenye shehia za Mchanga mdogo, Kinyikani, Kiungoni, Mjini ole, Kangagani na Shengejuu.
WANAKAMATI ya mradi wa GEWE III, waliohudhuria mkutano wa siku moja, uliozungumzia aina ya makosa ya udhalilishaji, uliofanyika uwanja wa Gombani Chakechake Pemba, ambapo mradi huo uko kwenye shehia za Mchanga mdogo, Kinyikani, Kiungoni, Mjini ole, Kangagani na Shengejuu, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.