Habari za Punde

ZIMAMOTO YAENDELEA KUVUTWA SHATI, KVZ YAREJEA KILELENI

Na Abubakar Khatib Kisandu, Zanzibar.
Ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja imeendelea tena 

leo kwa kupigwa michezo miwili katika uwanja wa Amaan 

ambapo saa 8 za mchana Zimamoto na Kipanga zilishindwa 

kutambiana baada ya kutoka sare ya kufungana bao 1-1.

Bao la Kipanga limefungwa na Nassor Ali wakati bao la Zimamoto likiwekwa nyavuni na Hassan Haji.

Saa 10 za jioni katika uwanja huo KVZ wakaitandika Polisi bao 1-0 kwa lililofungwa na Salum Songoro dakika ya 79.

Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa kupigwa mchezo mmoja katika uwanja wa Amaan saa 10:00 za jioni kati ya Jang’ombe boys dhidi ya Chuoni.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.