Habari za Punde

AFC Leopards wamtaka Mwinyi Haji Ngwali

Na Mwandishi wetu

Mchezaji wa timu ya Taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes ambae pia huichezea Timu ya Young Africans, Mwinyi Haji Ngwali huenda akahamia Timu ya AFC Leopards ya nchini Kenya endapo timu hizi mbili zitakubaliana.
Haji Mwinyi Ngwali ambae hucheza kama beki wa kushoto aling'ara sana katika mashindano ya CECAFA Challenge Cup yaliyomalizika karibuni Machakos, nchini Kenya ambapo Zanzibar iliibuka mshindi wa Pili.
Licha ya Timu yake ya sasa Yanga kutomtumia sana katika msimu huu mpaka kuikosa nafasi yake katika Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Haji Mwinyi alicheza kwa kiwango kikubwa katika mashindano ya CECAFA
Kwa mujibu wa mazungumzo yaliyofanyika kati ya mchezaji na AFC Leopard tayari wameshamalizana na wanatarajia mwishoni wa mwaka huu au mwanzoni mwa mwaka ujao atakuwa mchezaji halali wa AFC Leopards.
"Tunajua ni mchezaji mzuri, tunajua thamani yake ndio maana tunajitahidi kuisaka saini yake" Alisema m moja wa viongozi wa Timu ya AFC Leopards
AFC Leopards ni timu inayoshiriki katika mashindano ya CAF Confederation CUP

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.