Habari za Punde

Naibu Waziri wa Elimu atembelea skuli zilizoboronga katika mitihani ya Taifa kisiwani Pemba

 Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mh. Mmanga Mjengo Mjawiri akizungumza na Walimu, Wanafunzi na Kamati ya Wazee Skuli ya Chokocho katika Ziara Maalumu ya kuzitembelea Skuli zilizofanya vibaya katika matokeo ya mitihani ya Taifa. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafuzo ya Amali Zanzibar Mh. Abdalla Mzee na Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Mkoani Mh. Issa Juma Ali
Walimu, wanafunzi  Wajumbe wa kamati ya Wazee Skuli ya Chokocho na wadau mbali mbali wa Elimu kisiwani Pemba katika ziara maalumu ya Mh. Naibu waziri wa Elimu Mh. Mmaga Mjengo Mjawiri Skuli ya Chokocho.



Na Ali Othman, Pemba

Naibu waziri wa Elimu na Mafunzo ya amali Zanzibar Mh. Mmanga Mjengo Mjawiri amefanya ziara maalumu kisiwani Pemba ya kuzitembelea Skuli zilizofanya vibaya katika mitihani ya Taifa mwaka 2017.

Mh. Mmanga ameanza ziara hiyo Skuli ya Chokocho wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba ambayo nimiongoni mwa Skuli tano za mwisho kwamatokeo mabaya ya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2017.

Akionesha kutoridhishwa na matokeo hayo alipokutana na kamati ya wazee, walimu na wanafunzi wa skuli ya Chokocho katika ukumbi wa sSkuli hiyo, Mh. Mmanga amesema hali hiyo inasikitisha na Serikali haipendi kuona skuli zake zikifanya vibaya hasa kwa vile miundo mbinu kama vile maabara ipo.

Akipitia sababu mbali mbali zilizotajwa kua chanzo cha matokeo hayo mabaya kwa baadhi ya skuli alizowahi kutembelea kisiwani Unguja Mh. Mmanga amesema, kwa baadhi ya skuli sababu zilizotajwa ni utoro  wa wanafunzi na kutokujali masomo yao, ushiriki mdogo wa wazazi, mabadiliko ya mitaala na uhaba wa vifaa.

Hata hivyo Mh, Mmanga amesema katika ufundishaji mtu muhimu sana ni mwalimu hivyo amewataka walimu kufundisha kwa viwango bora, kupima kwa viwango sahihi na kutoa mrejesho kwa wakati.

Mh. Mmanga ameonya tabia ya baadhi ya walimu kutumika katika Skuli binafsi na kuacha kutekeleza ipasavyo majukumu yao katika Skuli za Serikali ambazo wameajiriwa.

“Tunazo taarifa kwamba baadhi ya walimu wanatumika katika skuli binafsi na hivyo utendaji wao unajikita zaidi katika Skuli hizo” Amesema Mh. Mmanga.

Awali naibu katibu mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mh. Abdalla Mzee akitoa tathmini ya matokeo hayo amesema Skuli ya Chokocho ni miongoni mwa Skuli tano za mwisho Zanzibar ambapo nne zipo Unguja.

Amesema kati ya wanafunzi 42 waliofanya mtihani Skuli ya Chokocho ni wanafunzi 10 tu waliofaulu na wengine 32 hawakufaulu. Akifafanua viwango vya ufaulu kwa wanafunzi  10 amesema, mwanafunzi 1 tu alipta daraja la pili, wanafunzi 2 walipata daraja la tatu na wanafunzi 7 walipata daraja la nne.





No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.