Habari za Punde

Mikononi mwa Polisi kwa tuhuma za kubaka mtoto wa darasa la pili



Na Salmin Juma , Pemba

Jeshi la Polisi mkoa wa kusini Pemba linamshikilia kijana wa miaka 16 mkaazi  wa Gombani  ya kale baada ya kudaiwa kumlawiti mtoto mdogo wa kiume wa miaka ( 10 ) ambae pia ni mwanafunzi wa darasa la pili na kumsababishia maumivu makali.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake madungu chakechake kamanda wa Polisi mkoa wa kusini Pemba  Shehan Mohd Shehan alisema tukio hilo limetokea jana majira ya saa 7:30 mchana huko Gombani ya Kale baada ya mashuhuda kubaini unyama huo.

Alisema mtoto huyo  aliagizwa na mamaake  kwenda kununua stika zake za mabuku na alipokua  akirejea kijana huyo alimkamata kwa nguvu na kumfunga mikono kisha kuanza kumalawiti.

“alimkamata kwa nguvu na kumpeleka vichakani, akamfunga mikono, kisha alianza  kumlawiti “ alisema Kamanda Shehan.
Kamanda Shehan alisema baadhi ya watu walisikia sauti za kelele kizitoka porini , walipoamua kwenda na ndipo kulipofanikisha kukamatwa kwa kijana huyo ingawa alijaribu kukimbia.

Shehan alisema, daktari amethibitisha kuwa mtoto huyo alilawitiwa , hivyo jeshi la Polisi linaendelea kukamilisha taratibu za kisheria ili kumfikisha mahakamani kijana huyo na sheria ichukue mkondo wake.

“hatutomuachia kwasababu amefanya kitendo cha kinyama sana,  jeshi la polisi mkoa wa kusini Pemba linalaani kwa nguvu zote juu ya tukio hili “ alisema kamanda

Kwaupande wake baba mzazi wa mtoto huyo (jina linahifadhiwa) alisema  , amehuzunishwa sana na tukio na hasa kuwa aliyetendewa tendo hilo ni mtoto wake wa kwanza .
“taarifa nilipata nikiwa wete , mkewangu mmoja yupo huko, mamaake huyu alinipigia na kunipa taarifa hii, niliumia sana , nilitoka mbio mpaka nyumbani  na kushuhudia hali hii “ alisema baba huyo.

Akizungumza kwa masikitiko huku akiangua kilio mbele ya waandishi wa habari baba huyo alisema, wazee wa mtuhumiwa wanamtumia rafiki yake ili amshawishi akubali mazungumzo na kuyamaliza kienyeji jambo ambalo alisema halitaki na hayupo tayari kufanya hivyo na anachotaka ni kuona sheria inachukua mkondo wake.

Nae Ust Rashid  Ali Rashid wa Ole Kichoni  alipoulizwa na mwandishi wa habari hizi juu ya vipi uislamu unavyolizungumzia  suala la liwati alisema,  jambo hilo limeharamishwa  katika uisilamu na  haitakiwi kabisa hivyo kwa yoyote mwenye kufanya tendo hilo ajue kuwa anafanya jambo baya ambalo Mungu lina mkasirisha.

“haifai kwa muislamu kumfanyia mwenzake liwati wala kumbaka, wito wangu kwa wananchi wajiepushe na matendo haya  kwani athari yake ni kubwa kimwili na hata kiakili, jamii ibadilike “ alisema Ust Rashid





No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.