Waziri
wa Fedha na Mipango Zanzibar Dkt. Khalid
Salum Mohamed akizindua Bodi ya Mamlaka ya Ununuzi na Uondoshaji Mali za
Serikali katika utekelezaji wa majukumu
ya kazi zao huko Mazizini Zanzibar.
Mwenyekiti
wa Bodi ya Mamlaka ya Uondoshaji Mali
za Serikali Zanzibar Abdulrahman
Mwinyi jumbe (kushoto) Mkurugenzi wa Bodi
ya Mamlaka ya Ununuzi na Uondoshaji Mali za Serikal Othman Juma Othman
wakimsikiliza Waziri wa Fedha na Mipango wakati alipokuwa akizungumza na
watendaji wa Bodi hiyo.
Waziri
wa Fedha na Mipango Zanzibar Khalid Salum Mohamed katikati akiwa katika Picha ya pamoja na
Wajumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Ununuzi na
Uondoshaji Mali za Serikal Zanzibar.
Picha Na Miza Othman Maelezo
–Zanzibar.
Na
Khadija Khamis –Maelezo
03/07/2018.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Khalid
Salum Mohamed ameitaka Bodi ya Mamlaka ya ununuzi na uondoshaji wa mali za Serikali
kufanya kazi kwa kuzingatia maadili na
kujenga uwadilifu katika kuhakikisha wanafanyakazi kwa mujibu wa sheria .
Hayo aliyasema leo huko katika
ukumbi wa Ofisi ya Takwimu Mazizini wakati wa uzinduzi wa Bodi mpya ya
Mamlaka ya ununuzi na uondoshaji wa mali
za Serikali.
Alisema
kufanyakazi kwa ufanisi na kuzingatia maadili kutasaidia kuweka misingi
madhubuti ya kazi na kuhakikisha fedha za Serikali zinalindwa na kusimamiwa
ipasavyo .
Aidha alisema wajumbe wa Bodi hiyo ndio
wasimamizi wakuu wa fedha za Serikali, hivyo iko haja ya kuhakikisha matumizi
ya fedha yanatumika kisheria na kuwepo usimamiaji
wa uhakika ili kuepukana na
ubadhilifu wa mali ya umma .
“Matumizi
yakienda kiholela holela kwa watendaji hatupati kitu lengo ni kuwapatia
maendeleo wananchi wetu katika sekta
mbali mbali za kiuchumi ,huduma za afya,
miundombinu ikiwemo barabara majengo makubwa ya Serikali, majengo ya skuli na kadhalika .”Alisema Dkt Khalid.
Alifahamisha ununuzi wa vifaa unachukua
fedha nyingi za Serikali katika ujenzi ,bidhaa
pamoja na huduma za wananchi hivyo ndio maana ikaanzisha
chombo hichi maalum cha kusimamia na kudhibiti matumizi ambayo huchangia
kuzorotesha maendeleo ya taifa .
Alieleza chombo hichi kisimamiwe na kutoa
muongozo katika masuala ya ununuzi wa bidhaa na kuhakikisha fedha iliyotumika
inalingana na kifaa ambacho kimenunuliwa ili kwenda sambamba na sheria .
“Tusipokuwa waadilifu katika dhamana ambazo
tumepewa tuhakikishe sisi ni wachache kulingana na kundi kubwa linalotutizama na tunauangamiza umma tuheshimu sheria na
taratibu zinazotuongoza pia tumuogope Mwenyezi Mungu ,”Alisema waziri wa fedha .
Nae Mwenyekiti wa Bodi hiyo Abdulrahman
Mwinyi Jumbe alisema ingawa mwanzo ni mgumu lakini atahakikisha
wanafanya kazi kwa uwadilifu na kuzingatia misingi ya sheria .
Alisema anaelewa kwamba nchi yetu iko
katika mageuzi makubwa ya kiuchumi hivyo itaendeleza kuleta mabadiliko ili
kuhakikisha yanapatikana maendeleo
endelevu katika huduma za wananchi .
Nae Mkurugenzi wa bodi hiyo Othmani Juma Othman amesema
atawajengea uwezo wafanyakazi kwa kuweza kuwapa mafunzo mbali mbali ya kielimu
ili kufanyakazi kwa ufanisi na kuacha kufanya kazi kwa mazowea .
Aidha alisema atahakikisha kila mfanyakazi anajulikana
kipato chake , hivyo iwapo akionekana maisha yake yamepanda kwa haraka hatua za
kisheria zitachukuliwa dhidi yake na wananchi watapewa elimu ya kuweza kutoa
taarifa za kipato hicho katika sehemu zinakohusika
No comments:
Post a Comment