Na.Abdi Shamna, Zanzibar.
SERIKALI ya
Mapinduzi ya Zanzibar imesema Umoja wa
Falme za Kiarabu (UAE) unalenga kufungua
Ubalozi mdogo hapa Zanzibar, kabla ya mwisho wa mwaka huu.
Hatua hiyo
itawezesha kuimarisha uhusiano wa Kidiplomasia kati ya nchi mbili hizo, zenye historia na ushirikiano a muda mrefu.
Hayo
yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi, Ussi Haji Ussi ‘Gavu’, katika Hoteli ya Park Hayyat mjini hapa,
wakati wataalamu kutoka UAE, walipokutana na Ujumbe wa Zanzibar, uliongozwa na
Waziri huyo.
Ujumbe huo
wa wataalamu 16 uliowasili nchini jana kwa ziara ya siku nne, umekuja nchini kwa
lengo la kukazia na kuandaa taratibu za utekelezaji wa yale yaliokubaliwa
kufuatia ziara ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,
iliyofanyika UAE, January, mwaka huu.
Akizungumza
na waandishi wa habari kabla ya kikao hicho maalum, Waziri Gavu alisema miradi mbali mbali kupitia sekta za Afya,
Mawasiliano, Elimu sambamba na ukuzaji
ushirikiano kati ay nchi mbili hizo, itajadiliwa.
Mapema Waziri
wa Nchi Ushirikiano wa kimataifa wa UAE Reem Ibrahim alisema, Umoja wa Falme za Kiarabu unakusudia
kuendeleza ushirikiano wa kihistoria uliopo kati ya nchi mbili hizo, kw maslahi
ay wananchi wake.
Alisema
kuwasili nchini kwa ujumbe wa UAE utawezesha nchi hiyo kufungua milango ya uwekezaji
kupitia sekta mbali mbali, ambapo utekelezaji wake unatarajiwa kufanyika katika
kipindi kifupi kijacho.
No comments:
Post a Comment