STATE
HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF
THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar
29.09.2018

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein leo amefanya uteuzi wa viongozi katika Taasisi mbali mbali za
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Kwa mujibu wa Taarifa
kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu
Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, Rais Dk. Shein amemteua Dk. Abdulla
Mohamed Juma kuwa Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii ambaye anachukua
nafasi ya Dk. Vuai Idd Lila ambaye atapangiwa kazi nyengine.
Katika uteuzi huo pia,
Rais Dk. Shein amemteua Khalfan Sheikh Saleh kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala
wa Serikali wa Uchapaji na Mpigachapa Mkuu wa Serikali, ambaye anachukua nafasi
ya Mohamed Suleiman Khatib ambaye atapangiwa kazi nyengine.
Aidha, Rais Dk. Shein
amemteua Said Juma Ahmada kuwa Mkurugenzi wa Baraza la Manispaa ya Mjini
Unguja, Mkurugenzi huyo wa Manipaa ya Mjini Unguja anachukua nafasi ya Aboud
Hassan Serenge ambaye anastaafu kwa mujibu wa Sheria.
Pia, Rais Dk. Shein
amemteua Amour Ali Mussa kuwa Mkurugenzi wa Baraza la Manispaa ya Magharibi
“A”, Amour Ali Mussa anachukua nafasi ya Said Juma Ahmada ambaye amehamishiwa
Manispaa ya Mjini.
Sambamba na hayo, Rais
Dk. Shein amemteua Ali Abdulla Said Natepe kuwa Mkurugenzi wa Baraza la
Manispaa ya Magharibi “B”, Ali Abdulla Said Natepe anachukua nafasi ya Amour
Ali Mussa ambaye amehamishiwa Manispaa ya Magharibi “A”. Uteuzi huo unaanza
tarehe 1 Oktoba, 2018.
Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax:
024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment