Mkurugenzi wa Utawala wa Tume wa Utumishi wa Walimu Moses Chitanda, alipokuwa akifungua mafunzo ya OPRAS kwa Maafisa Elimu wa Mkoa wa Manyara jijini Dodoma.
Mwakilishi kutoka Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta ya Umma, PS3 Geoffrey Lufumbi, akitoa maelezo ya utangulizi na jukumu la mradi huo wakati wa mafunzo hayo ya OPRAS
Na Atley Kuni- OR
TAMISEMI
Imeelezwa kuwa moja
ya njia itakayowezesha taifa liweze kupiga hatua katika nyanja mbali mbali za
maendeleo ni kwa taifa hilo kujiwekea mazingira ya kupima utendaji wa kazi kwa
njia iliyo wazi na inayotoa nafasi kwa mtumishi kujitathmini mwenyewe.
Kauli hiyo imetolewa
na Ndg Moses Chitanda (kwa niaba ya Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu Bibi
Winfrida Rutaindurwa) kwenye mafunzo ya siku mbili kwa Maafisa Elimu wa Mamlaka
za Serikali za Mitaa juu ya mfumo wa (Open Performance Review Appraisal System-OPRAS)
kwa Mkoa wa Manyara yanayofanyika jijini Dodoma.
Ndg Chitanda alisema
mataifa mengi yaliyoendelea yaliwekeza katika rasilimali watu ikiwemo katika kupima
na kufanya tathmini, na hii imewezesha mataifa hayo kupiga hatua za kimaendeleo.
Chitanda alisema,
kujituma, nidhamu sambamba na kupokea maelekezo ndio njia pekee inayomwezesha
mtumishi wa umma kupiga hatua katika utendaji wake wa kazi.
Mkurugenzi huyo wa
rasilimali watu kutoka Tume ya Utumishi wa Walimu alifafanua, katika hali ya
sasa nchi inahitaji watu wabunifu na wachapa kazi ambao watapatikana kwa
rasilimali watu kutekeleza mfumo wa OPRAS.
“Mafunzo haya ya
OPRAS yatasaidia kuibua ubunifu na utendaji uliotukuka hivyo tutegemee matokeo
chanya kwa walimu”.
Chitanda alisema,
shabaha kuu ya kuanza na kada ya walimu kwenye kuboresha ujazaji wa malengo ya OPRAS
ni kutokana na kundi hilo kuwa na majukumu mengi yanayo fanana lakini pia weledi
na wepesi wakusaidia kuisambaza elimu hiyo kwa makundi na kada zingine.
“Ili kuwa na utekelezaji wa uhakika wa
utaratibu ulioboreshwa, wadau walikubaliana kuchagua kada moja katika utumishi
wa umma ili liwe kundi la kuanzia, kwa kutumia vigezo mbalimbali, alisema
Chitanda na kuongeza ilikubaliwa zoezi lianzie kwa walimu ambao kwa mujibu wa
kazi zao ni lenye majukumu ya aina moja ambayo yanaweza kupangwa kwa kutumia
maelezo ya kazi ya kada ya walimu”.
Lakini pia ni rahisi kueneza elimu hii mpya ya upangaji malengo ya
mtumishi”.
Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Mradi wa
Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta ya Umma, PS3 Geoffrey Lufumbi, alisema mafunzo
hayo ni mwanzo wa mafunzo yanayotolewa nchi nzima kwa Mikoa na Mamlaka za
Serikali za Mitaa na kufuatiwa na walimu wote nchini.
Ndg Lufumbi alibainisha kuwa zoezi hili
limefanikiwa kwa ushirikiano uliopo baina ya Serikali kupitia Ofisi ya Rais-TAMISEMI,
Tume ya Utumishi wa Walimu na PS3 kama sehemu mojawapo ya uimarishaji wa mifumo
ya Rasilimali Watu kupitia Mradi wa PS3.
“Maamuzi yote ya taasisi ikiwepo upangaji
wa kazi na watumishi yatafanikiwa tu endapo OPRAS zitajazwa kwa ufasaha na
itasaidia kutambua malengo kama yamefikiwa ama la”.
“Kama PS3 tunafanya kazi katika vipengele mbalimbali
ikiwepo Utawala Bora, Mifumo ya TEHAMA, Mifumo ya Fedha, Tafiti tendaji pamoja
na Rasiliamali Watu.
Akitoa mada katika kwenye mafunzo hayo ya
siku mbili, mmoja ya wawezeshaji wa kitaifa wa OPRAS Ndg Samson Medda, alisema
Mipango, malengo, dira na dhima ya taasisi vitafanikiwa kwa taasisi kuwa na
OPRAS inayotekelezwa kwa umakini.
Katika Semina hiyo Ndugu Chitanda hakuacha
kuwashukuru Watu wa marekani kupitia mradi wa uimarishaji wa mifumo ya sekta za
umma PS3 kwa kazi kubwa wanayoifanya nchini yakuwezesha mifumo mbali mbali
hususan ni imarishaji wa Mifumo ya Sekta ya Umma.
Mpango wa watumishi kwa njia ya wazi
umefafanuliwa kupitia, Miongozo na
Sheria mbali mbali za utumishi wa umma ikiwepo Sheria ya Utumishi wa Umma ya Mwaka
2007 kupitia Kifungu cha (3) cha marekebisho Namba 18 ya 2007 kinafafanua dhima
ya Makatibu Wakuu, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Taasisi zinazojitegemea
pamoja na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kutumia fomu za OPRAS katika
kupima utendaji wa watumishi waliopo chini yao.
No comments:
Post a Comment