Habari za Punde

MASAUNI: TUTADHIBITI UHALIFU MAENEO INAKOPITA MIRADI YA SERIKALI

Naibu  Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza katika  kikao  cha ndani  kilichojumuisha Kamati  ya  Ulinzi  na  Usalama  ya  Wilaya  ya Manyoni  wakati  wa ziara  ya  kikazi, lengo ikiwa ni kuweka mikakati ya  kudhibiti hujuma na  uhalifu katika maeneo inapopita miradi mbalimbali ya serikali. Naibu Waziri yuko mkoani Singida kwa ziara ya kikazi
Naibu  Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati mstari wa mbele), akiongozana na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Manyoni kuingia katika  Kituo cha Polisi cha Manyoni kinachojengwa baada ya kituo cha awali kupitiwa na Mradi   wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa . Naibu Waziri yuko mkoani Singida kwa ziara ya kikazi
Muonekano wa nje Kituo Kipya cha Polisi Wilaya ya Manyoni ambacho kipo mbioni kukamilika ambacho kinategemewa kudhibiti hujuma na uhalifu katika maeneo mbalimbali inakopita miradi mikubwa ya serikali
Naibu  Waziri  wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(wapili kushoto), akiangalia ramani ya eneo linarotarajiwa  kuejngwa kituo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.Wengine ni Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wilayani Manyoni  Naibu Waziri yuko mkoani Singida kwa ziara ya kikazi. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Na Mwandishi Wetu
Serikali  iko  katika  mpango  wa  kujenga  Kituo  cha  Polisi  katika Halmashauri  ya  Itigi ikiwa  ni  juhudi  za  kulinda  hujuma  na  uhalifu  katika  Ujenzi wa Reli ya Kisasa (Standard Gauge)  na  Mradi  wa  Umeme katika maporomoko ya maji ya Mto Rufiji (Stiegler’s Gorge) baada ya wavamizi  kuingia eneo la hifadhi ya Rungwa ambayo kuna mito 18 ambayo ni chanzo   cha Mto Rufiji ambako mradi wa umeme unajengwa.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni akitembelea na kukagua Mradi wa Kituo kipya cha Polisi cha Wilaya ya Manyoni na kukagua eneo linarotarajiwa kujengwa Kituo cha Polisi Itigi lengo ikiwa kudhibiti matukio ya uhalifu.
Akiambatana   na  Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Manyoni, Naibu Waziri Masauni amesema Serikali iko tayari kutumia mbinu mbalimbali kuhakikisha miradi mikubwa ambayo Serikali ya Awamu ya Tano imeianza inakamilika bila kufanyiwa hujuma zozote na wahalifu.
“Miradi  mikubwa ambayo Rais wetu  Dkt. John Magufuli na serikali anayoiongoza ameianzisha  ni  muhimu  ikalindwa ili ilete manufaa kwa nchi pindi  itakapokamilika  na sisi  kama wizara  tutahakikisha  tunasogeza  huduma za  Ulinzi na  Usalama  katika maeneo  yote  ambayo  miradi  hiyo inapitia, ndio maana leo nimetembelea ujenzi wa Kituo cha Polisi Manyoni ambacho kiko mbioni kukamilika  lengo ikiwa ni kulinda miradi hiyo mikubwa,” alisema Masauni
Akizungumza  katika  ziara hiyo,  Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki, Daniel  Mtuka amekiri  kuwepo  na  haja  ya  kituo  katika  Wilaya  za  Manyoni na  Itigi  ili  kuweza kuboresha  usalama  katika  maeneo  hayo  ambayo yanapitiwa  na  miradi  hiyo  mikubwa miwili  huku  akiiomba wizara kuleta askari  katika  vituo  hivy pindi ujenzi utakapokamilika.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.