Habari za Punde

Serikali yaweka mikakati kuhakikisha mapato yanaongezeka


Na Takdir Ali,                             7-01-2019.

Waziri Wa Fedha Na Mipango Dkt,Khalid Salum Muhammed amesema serikali imeweka mikakati ya kuhakikisha mapato ya serikali yanaongezeka na kuziba mianya yote inayoashiria kuvuja kwa mapato.

Amesema ukusanyaji wa mapato ni nzuri lakini bado kuna 
baadhi ya watu wachache wananakwenda kinyume na taratibu zilizowekwa na kuwataka wenye tabia hizo kuacha mara ili kujiepusha na matatizo yanayojitokeza.

Ameyasema hayo huko Bandarini Malindi mara baada ya kumaliza ziara iliowashirikisha Waziri Wa Fedha Na Mipango,Waziri Wa Biashara Na Viwanda Na Waziri Wa Ujenzi,Mawasiliano Na Usafirishaji kufuatia kuibuka malalamiko katika Baraza La Biashara ambapo mwenyekiti wake ni Raisi Wa Zanzibar Na Mwenyekiti Wa Baraza La Mapinduzi Dkt Ali Muhamed Shein.

Amesema walipofanya baraza la pili la biashara viongozi wa taasisi binafsi walizungumzia matatizo ya uendeshaji wa bandari,miondombinu duni,na kutoingia kwa makontena kutoka mombasa mamboa ambayo yanpaswa kupatiwa ufumbuzi wa haraka ili kuwaondoshea usumbufu wananchi.

Amesema ziara hiyo imekuja kufuatia raisi wa zanzibar kuzitaka taasisi zote zinazohusika wakutane na wafanyabiashara ili tatizo hilo liweze kupaiwa utatuzi wa haraka sana.

Hata hivyo amewataka watendaji hao kutokubali kurubuniwa na baadhi ya watu wachache wasioopenda maendeleo ya nchi na kutoa wito kwa wenye tabia hiyo kuacha mara moja.

Kwa upande wake Waziri wa Ujenzi Mawasiliano Na Usafirishaji Dkt.Sira Ubwa Mwamboya amesema mategemeo ya serikali yapo mikononi mwao hivyo ni vyema kufanya kazi kwa ukweli ili kuweza kukusanya mapato vizuri na kuiwezesha serikali kuhudumia vizuri wananchi wake.

Amesema wafanyabiashara wanakuwa wanaangalia maslahi katika biashara zao hivyo nio vyema kutoshirikiana na wafanyabiashara wasiokuwa waamini fu ili kuepukana na ubadhirifu unaoweza kujitokeza.

Nae Naibu Kamishna Wa Mamlaka Ya Mapato Zanzibar (Tra) Mcha Hassan Mcha ameahidi kuyafanyia kazi maagizo waliopewa ili kuhakikisha mapato ya serikali wanayokusanya yanaongezeka.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.