Habari za Punde

Kutoka Bungeni Jijini Dodoma leo.

Wanafunzi wa shule ya msingi Mzakwe ya Jijini Dodoma wakiwa mbele ya ukumbi wa Bunge leo Jijini Dodoma.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kangi Lugola, akiwasilisha hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake leo bungeni Jijini Dodoma. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Kangi Lugola, akisisitiza jambo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (katikati) leo Bungeni Jijini Dodoma.
Naibu Waziri Wizara ya Nishati, Mhe. Subira Mgalu, akisisitiza kuhusu hatua zinazochukuliwa na serikali katika kuhakikisha kuwa gesi inawafikia wazalishaji  katika viwanda vyote vilivyopo katika ukanda unaopitiwa na bomba hilo kati ya Mtwara na Dar es Salaam kulingana na maombi ya kuunganishiwa huduma hiyo.
Katibu mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu,(wakwanza kushoto) akifuatilia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi wakati Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Kangi Lugola akiwasilisha hotuba hiyo leo Bungeni  Jijini Dodoma.
Naibu Waziri Ujenzi Uchukuzi na Mawasilaino, Mhe. Atasashta Nditiye, akitoa ufafanuzi kuhusu kuanza kwa zoezi usajili wa laini za simu kwa kwa kutumia alama za vidole na kitambulisho cha taifa. Zoezi hilo linatarajiwa kuanza mwezi Mei na kukamilika mwezi Disemba 2019.

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, mhandisi Hammad Masauni, akisisitiza kuhusu askari wa kikosi cha usalama barabarani kuzingatia sheria kanuni na taratibu wanapotekeleza majukumu yao  leo  Bungeni Jijini Dodoma.

(Picha zote na Frank Mvungi- MAELEZO)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.