Habari za Punde

Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi CP Liberates Sabas, Ameteta na Wananchi wa Kijiji cha Rungungu (RUFIJI) na Kufanya Operesheni Kali Katika Makazi Yaliotumiwa na Wahalifu Kipindi Cha 2016/2017.

 
Kamishna wa Opereshni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi CP Liberates Sabas, akizungumza na wanakijiji cha Rungungu baada ya kuwatembelea na kutaka kujua maendelea yao na Usalama wa Kijiji hicho, hatua hiyo ya kuwatembelea wanakijiji hao kamishna CP Sabas  huifanya mara kwa mara kwasababu ya kijiji hicho ndicho kilikuwa makazi makuu ya wahalifu pamoja na eneo walilokuwa wakifanyia mafunzo yao kabla ya kutimiza azima zao katika kipindi cha miaka ya 2016 na 2017. 
Kamishna wa Opereshni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi CP Liberates Sabas, akiwa katika picha ya pamoja na askari wa kikosi maalum cha kupambana na wahalifu katika pori la Rungungu liliopo Kijiji cha Rungungu katika Mkoa wa Kipolisi Rufiji baada ya kumaliza kufanya Operesheni maeneo hayo. 

Kamishna wa Operesheni na Mafunzo ya Jeshi la Polisi CP Liberates Sabas, akikagua mradi wa ujenzi wa Nyumba za Askari Polisi uliofadhiliwa na Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, katika eneo la Ikwiriri, Mkoa wa Kipolisi Rufiji na kulidhishwa na maendeleo mazuri ya ujenzi huo. ( Picha na Jeshi la Polisi )

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.