Habari za Punde

Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein Atembelea Wazee wa Seblenina Welezo na Watoto wa Kijiji cha SOS na Mazizini Zanzibar Kutowa Mkono wa Eid Fitry leo.NA


Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akiwasalimia na kutowa Mkono wa Eid Fitry, kwa Wazee wa Nyumba ya Wazee Sebleni Zanzibar, alipofika kuwatembelea leo  akiwa na Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleima Iddi.  

WATOTO wanaoishi katika nyumba za kulelea watoto katika kijiji cha SOS na Mazizini, Mkoa Mjini Magharibi Unguja, wametakiwa kuwa makini na wasikivu katika kipindi hiki cha kuelekea sikukuu za Eid el Fitri ili kuepukana na vitendo hatarishi.

Indhari hiyo imetolewa na Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na watoto Moudline Castico, kwa wakati tofauti alipokuwa akitowa shukrani kwa Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein na Mke wa Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mama Asha Suleiman Idd, baada ya kukamilika hafla ya utowaji wa zawadi za Sikukuu kwa wazee wanaotunzwa na Serikali, nyumba za wazee  Welezo, Sebleni pamoja na watoto wanaolelewa katika vituo vya SOS na Mazizizni.

Aliwataka watoto hao kuwa wasikivu wakati wanapokwenda na kurudi katika viwanja vya sikukuu pamoja na kufuata maelekezo ya wakubwa zao, ili kuepukana na matukio mbali mbali yanayoweza kuhatarisha usalama wao.

Alisema ni vyema kuwa pamoja wakati wote wa sikukuu na kufuata malekezo yanayotolewa.

Aidha, Waziri Castico aliwapongeza viongozi hao kwa kuendeleza utamaduni wa kuwatembele na kuwapa zawadi wazee na watoto hao kila nyakati za sikukuu zinapofika.

Alieleza kuwa hatua hiyo inaendeleza imani na upendo kwa wazee na watoto hao.

Nae, Mkurugenzi wa Ustawi wa Jamii Zanzibar, Wahida Maabad aliwashukuru viongozi hao kwa kuendeleza utamaduni wa kuwapatia futani na zawadi za sikukuu wazee na watoto hao

Alisema hatua hiyo inawapa faraja na kuamini kuwa ni sehemu ya jamii ambayo inathaminiwa.

Katika hafla hiyo jumla ya wazee 37 kutoka nyumba za kutunzia wazee Welezo walizawadiwa, sambamba na wazee 35 wanaoishi katika nyumba za wazee Sebleni.

Aidha, watoto 35 wanaoishi katika  nyumba ya kulelea watoto Mazizini pamoja na watoto 180 wanaoishi atika Kijiji cha kulelea watoto SOS walizawadiwa.

Katika mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, kwa nyakati tofauti viongozi hao walipata fursa ya kufutari pamoja na watoto wa vituo vya SOS na Mazizini, ikiwa ni utaratibu wao wa kila mwaka.

Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822 
 E-mail: abdya062@gmail.com

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.