Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Issa Haji Gavu. akizungumza na kutowa shukrani kwa Wananchi waliohudhuria hafla ya futari ilioandaliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, katika viwanja vya Ikulu Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk.Ali
Mohamed Shein amewataka waumini wa Dini ya Kiislamu nchini kuendeleza upendo
na mshikamano, ili kuimarisha dini hiyo pamoja na kupata fadhila kutoka kwa
Mwenyezi Mungu.
Dk.
Shein amesema hayo katika viwanja vya Ikulu mjini hapa baada ya kukamilika
hafla ya futari, aliyoiandaa kwa wananchi wa Mkoa wa Mjini Magharibi.
Akitoa
neno la shukurani kwa niaba yake, Waziri wa Nchi (OR) na Mwenyekiti wa Baraza
la Mapinduzi, Issa Haji Ussi Gavu alisema mshikamano na upendo miongoni mwa
waumini huleta maelewano na kuwa chachu katika uimarishaji wa dini hiyo.
Alisema
hatua hiyo hufanikisha dhamira ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, na hivyo waumini
kupata fadhila kubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu.
Alisema
utaratibu wa kila mwaka wa Rais Dk.
Shein wa kujumuika pamoja na wananchi katika
futari una mnasaba na dhamira hiyo, hivyo akabainisha matumaini yake
ya utamaduni huo kuendelelea mwakani.
Aidha,
alitowa shukurani kwa wananchi wote walioshiriki katika hafla hiyo, na kusema
hatua waliyoionyesha ya kuwacha familia zao inaonyesha heshima na mapenzi makubwa waliyonayo kwa kiongozi huyo.
Waziri
Gavu aliwatakia kheri wananchi hao katika kukamilisha mfungo wa mwezi wa
Ramadhani sambamba na maandalizi mema ya sikukuu ya Idd el Fitri.
Abdi Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024
2231822
E-mail:
abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment