Habari za Punde

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Simbachawene Akiendelea na Ziara Yake Zanzibar.



Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. George Boniface Simbachawene (kushoto) akizungumza na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Mohamed Aboud (katikati) alipomtembelea Ofisini kwake Vuga kujitambulisha. Kulia ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mhe. Mihayo Juma Nunga

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Mohamed Aboud akimuonesha maeneo mbalimbali ya Mji wa Zanzibar Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. George Boniface Simbachawene baada ya kumtembelea na kufanya nae mazungumzo Ofisini kwake.
Mratibu wa Shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Khalid Bakari Hamrani (wa pili kulia) akimpa maelezo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. George Boniface Simbachawene kuhusu ujenzi unaoendelea wa jengo la Kituo cha Afya Kianga Wilaya ya Magharibi A Mkoani Mjini Magharibi unaojengwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) na kusimamiwa na wananchi wenyewe. Kulia ni Mkurugenzi wa Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais Lupi Mwaikambo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. George Boniface Simbachawene akikagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kianga Wilaya ya Magharibi A Mkoani Mjini Magharibi unaojengwa kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) na kusimamiwa na wananchi wenyewe.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. George Boniface Simbachawene akizungumza alipotembelea eneo la Kilimani mjini Zanzibar kwenye mradi wa miti ya mikoko kando ya Bahari ya Hindi ili kuhifadhi mazingira ikiwa ni sehemu ya ziara yake. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Farhat Ali Mbarouk.
HABARI NA PICHA ZOTE KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.