Habari za Punde

Rais Mstaafu wa Tanzania Mhe.Benjamin Mkapa Aongoza Mhadhara wa SADC Jijini Dar es Salaam leo.

Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Benjamini William Mkapa akihutubia katika mhadhara uliofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) uliokuwa ukizungumzia historia ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), mapema leo Agosti 15, 2019.  Majaji wastaafu wakiwa na Katibu Mkuu wa CCM, Bashiru Ali (picha ya juu Kulia) waliohudhuri mhadhara wa uliongoongozwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Benjamini Wiliam Mkapa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) uliokuwa ukizungumzia maendeleo ya nchi za Jumuiya za Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) mapema leo Agosti 15, 2019.
Katibu Mkuu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Dkt. Stagomena Tax akizungumza katika mhadahara uliokuwa ukielezea historia na jinsi SADC ilivyoweza kusonga mbele, mapema leo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).


Waziri wa Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibarv Mhe, Mahmoud Thabit Kombe, (kushoto ) akizungumza na Viongozi walioohudhuria Mhadhara wa SADC katikati Waziri wa Katiba na Sheria Zanzibar Mhe Khamis Maalim Juma. 
 Mabalozi, Mawaziri na viongozi wa nchi mbali mbali waliohudhuria Mhadhara huo. Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt Harrison Mwakyembe aliyemuwakilisha Waziri wa Mambo ya Nje ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof Palamagamba Kabudi akitoa machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Rais Mstaafu Mkapa.

 Salamu za hapa na pale...
Wimbo wa Taifa ukiimbwa...
Wageni waalikwa.
Meza kuu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.