Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mwakilishi Mkaazi na Mratibu wa Mashirikaka ya Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Bwana.Alvaro Rodriguez,alipofika Ikulu Zanzibarv leo, kwa mazungumzo na kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi Tanzania.
UMOJA wa Mataifa (UN) umeahidi kuendelea kuiunga
mkono Zanzibar katika kuhakikisha miradi yote ya maendeleo inayosimamiwa na
Mashirikia yake inatekelezwa kikamilifu na kupata mafanikio kwa azma ya
kuwasaidia walengwa ambao ni wananchi wa Zanzibar.
Mwakilishi Mkaazi na
Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa (UN) hapa Tanzania Alvaro Rodriguez
alisema hayo leo wakati alipofika Ikulu kwa ajili ya kuaga na kufanya
mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali
Mohamed Shein.
Alieleza kuwa Mashirika
yote ya Umoja wa Mataifa (UN) yanayofanya kazi zake hapa Tanzania yanapongeza
juhudi zinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya uongozi wa
Rais Dk. Shein na kuahidi kuendelea kuunga mkono kwani wanafarajika na juhudi
hizo.
Alieleza kuwa Umoja wa
Mataifa (UN) unapongeza sana juhudi hizo za Rais Dk. Shein na unaahidi kuendelea
kushirikiana nae huku akieleza kuwa mashirika yote ya (UN) yana matumaini
makubwa ya kuona matokeo endelevu yatakayotokana na juhudi hizo katika miaka
ijayo.
Pia, kiongozi huyo
alieleza azma ya Mashirika hayo ya UN katika kuendelea kuunga mkono juhudi za
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuimarisha miradi ya maendeleo ikiwemo
elimu, afya, upatikanaji wa maji safi na salama, utawala bora, uimarishaji wa
haki za binaadamu, uwezeshaji, mapambano ya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake
na watoto uhifadhi wa mazingira pamoja na mambo mengineyo.
Mratibu huyo alieleza
mafanikio yanayopatikana ambayo yamepewa kipaumbele katika utekelezaji wa ‘Programu ya pamoja ya Zanzibar
ya mwaka 2018-2021’ iliyozinduliwa Agosti mwaka jana yakiwemo kupunguza vifo vya uzazi, ukatili
dhidi ya wanawake na watoto, uwezeshaji wa kiuchumi kwa wanawake kupitia zao la
mwani pamoja na uratibu wa utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).
Mratibu huyo alieleza
kuwa licha ya yeye kupangiwa majukumu mengine ya kikazi lakini anaamini kwamba
kiongozi atakaye chukua nafasi yake ataendeleza uhusiano na mashirikiano mema
yaliopo kati ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na UN.
Nae Rais Dk. Shein kwa
upande wake alitoa pongezi kwa Umoja huo chini ya Mratibu wake hapa Tanzania
Alvaro Rodrigues ambaye amemaliza muda wake wa kazi hapa nchini kwa kuendelea
kushirikiana na kuiunga mkono Zanzibar katika kuendeleza miradi mbali mbali ya
maendeleo.
Rais Dk. Shein alieleza
kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na wananchi wake wanampongeza Mratibu
huyo kwa kuonesha moyo na juhudi kubwa za kuisaidia Zanzibar na kuiunga mkono
katika miradi yake ya maendeleo wakati wa uongozi wote wa Rodrigues alipokuwepo
nchini.
Aidha, Rais Dk. Shein
alimtakia safari njema Mratibu huyo na kumtaka akaendelee kuchapa kazi kwa
juhudi na maarifa kama alivyofanya wakati akiwa hapa Tanzania.
No comments:
Post a Comment